Thursday, November 26, 2015

YATUPASA KUSHUKURU
Ndugu yangu sikiliza,kwani naanza eleza,
Si vema kuyapuuza,haya ninayokueleza,
Yapasa kumpendeza,yeye aliyetukweza,
Upendo wa mungu kwetu,yatupasa kushukuru.
Ibada ni ya muhimu,kumshukuru rabuka,
Kumsifu si hukumu,kwani anatukumbuka,
Kumsujudu kwa hamu,ndipo anaporizika,
Upendo wa mungu kwetu,yatupasa kushukuru.
Tumpende kwa hakika,si vema kusuasua,
Ndipo tupate baraka,ambazo hutupatia,
Nivema kumkumbuka,yeye atupendelea,
Upendo wa mungu kwetu,yatupasa kushukuru.
Vitabu vyake kusoma,tupate yake kushika,
Amri zake kusoma,kusudi kuzikumbuka,
Yeye ni mwenye hekima,kwani amekamilika,
Upendo wa mungu kwetu,yatupasa kushukuru.
Tumshukuru rabuka,mapenzi yake kutupatia,
Na mwisho kwake kufika,tupate kufurahia,
Nitaona malaika,mungu kimsujudia,
Upendo wa mungu kwetu,yatupasa kushukuru.
Tamati namalizia,mambo hayo zingatia,
Kwa kumshukuru pia,kwa uhai tupatia,
Iabuda kumufanyia,jambo hilo ni sawia,
Upendo wa mungu kwetu, yatupasa kushukurU



No comments:

Post a Comment