Sunday, November 29, 2015

MAPENZI TUYAPE PUMZI


MAPENZI TUYAPE PUMZI

Tuanze kama safari,twende mbali tukaone,

Mapenzi yetu hatari,nimeshazama nione,

Nitakupa hata gari mapenzi yetu yanone.

Mapenzi tuyape pumzi,yapumue kwa furaha.

 

Mapenzi tuyape pumzi yapumue kwa furaha,

tusije kuwa machizi,tukaishi kwa karaha,

tusifanye kama wezi,tupumue kwa furaha,

Mapenzi tuyape pumzi,yapumue kwa furaha.

 

Nakupenda si utani,usiniache jamani,

Penzi lako chini chini,nitulize kivulini,

Tusiyachome juani,tukajuta maishani,

Mapenzi  tuyape pumzi yapumue kwa furaha.

 

Usiwafate mabuzi,wakakuchuna na wewe,

Ukafanana na mbuzi,na sura mbaya ya mwewe,

Penzi letu ni mchuzi ,nimedata kwako wewe,

Mapenzi tuyape pumzi,yapumue kwa furaha.

 

Jamani kipenzi changu,ninakupenda moyoni,

Asali ya moyo wangu,sasa  shubiri ya nini?,                                  

Niponye nafasi yangu,nakupenda si utani,

Mapenzi tuyape pumzi,yapumue  kwa furaha.

 

Sina kinyongo moyoni,wala kiburi usoni,

Furahaa yangu machoni ,kicheko changu kinywani,

Papaso lako mwilini, lanipa joto jamani

Mapenzi tuyape pumzi yapumue kwa furaha.

No comments:

Post a Comment