Thursday, November 26, 2015

HADITH YA PILI


“NILITEMBELEWA NA MALAIKA”

Sura ya kwanza

Kwenye kijito cha maji

Ilikua  Yapata saa nane na nusu  mchana siku ya juma mosi mwezi  desember tarehe 25 mwaka 2010 ilikua ni siku nzuri sana kwa upande wangu,sio tu kwa upande wangu nadhani labda hata kwa watu wengine wengi waliopo duniani, kwani tarehe hiyo  katika historia ya dunia ni tarehe maalumu na muhimu kwa ajiri ya  kusherehekea kufurahia,kushangiria na kuburudikia  sherehe ya kuzaliwa kwa bwana wetu na mwokozi wetu yesu kristo mwana wa pekee kwa mungu baba kama imani ya wkristo wengi duniani ilivyo.

Hali ya hewa ilibadirika ghafra kukawa mkusanyiko  na mawingu mawingu meusi meusi yaliyo ambatana na upepo mkubwa kiasi ulio kua ukivuma kwa madaha na maringo kwa hali kama ile wahenga wetu walisema dalili ya mvua ni mawingu,naam mvua ilikua inataka kunyesha na mvua ya siku ile haikua mvua ya kitoto bali ni mvua ya nguvu. Kila mtu aliye yazoea  majira ya mwezi desember haswa haswa kipindi cha sherehe za chirstmass alitegemea na alitarajia kwamba mvua kubwa kama ile ingenyesha tu kwani ndio kawaida ya mvua hizi kunyesha huku kwetu Mbeya  na kufanya mito na vijito kufurika maji machafu yaendayo safari za mbali kusiko julikana.

Watoto wengi wa matajiri walitia fora siku ile kwa kuvaa viwalo vipya vya bei gharama sio tu watoto wa matajiri na hata wale wanaotoka katika familia za hali ya chini hawakua nyuma kujichagulia viwalo mbali mbali katika mabanda ya nguo   za mituumba nguo maarufu sana huku kwetu mbeya, kwani hizi ni nguo zenye sifa ya kipekee  sana hizi ni nguo zinazo aminika kuwaziliwahi  tumika au ziliachwa  na wazungu wa huko ulaya au nchi nyingine zenye viwanda ili ziuzwe  kwa bei ya chini.

Ni hali kawaida sana kwa watoto kupenda kuvaa nguo mpya kila msimu wa sikukuu hizi za  Noeli na mwaka mpya,tofauti na watu wazima ambao wamezoea kuvaa kikawaida kawaida tu kwani wao awana shida na mavazi kwao mavazi ni kila siku hununua na kuyavaa mapyakwa mtindo wa kubadirisha badirisha.Sherehe zilinoga zikanogera,zilipendeza zikapendeka,zilivutia zikavutika, watu walikunywa,walikula na kusaza,watu wengine walitembea au kutembelehana na kupeana zawadi pamoja na heri ya Noeli.

wakiusubiria mwaka mpya kwa hamu kuu mfano wa wanawali sita walio hadithiwa katika kitabu cha mathayo;       wakimgoja bwana harusi ambaye ni yesu hata pale alipotokea walifurahi pamoja  na kufanya sherehe.hapo ndipo tunapaswa kutambua kua imetupasa kusubiri kwani subira yavuta heri  na iwapo tutakua na haraka haraka tutakosa Baraka.

 

 Mara baada ya mimi kupachika kinywani mwangu  matonge mawili matatu ya pilau na nyama ya  kuku pamoja na juice ya embe  lenye mchanganyiko wa  carrot na matango nilijisikia kushiba kwa kiasi kikubwa palenyumbani kwetu Nikanyanyuka kiuvivu uvivu kutoka kwenye kigoda,kigoda alichozoea kukikalia bibi yangu   aliye mzaa mama yangu, na baada ya kujinyanyua taaratibu niliingia chumbani kwangu na hata nilipo fika ndani ya kile kijumba nyasi chetu  utusi tusi na giza giza la mule chumbani vilinifanyanishindwe kuliona vema gitaa langu nililolilihifadhi kwenye kona ya chumba changu cha kulala karibu karibu na kitanda changu  nadhifu kinachonipendeza.

Nilianza kupapasa papasa ukuta ili kuelekea eneo ambalo gitaa langu lilikuwepo na kwa bahati nzuri mikono yangu iliweza  kuligusa na kulichukua  na kisha baada ya kutoka nje ya kile chumba changu kizuri kinachonipendeza,najivunia kusema kuwa chumba  changu knanipendeza kwa sababu ni cha kwangu na pia binafsi nakipenda kwani sio mbaya mtu kukipenda au kuipenda mali yake hapo ndipo ule usemi wa chako ni chako cha mtu sio chako au ule usemi usemao kipende sana chako kwani cha mtu ni mavi semi hizi zinaambatana na ile semi niipendayo sana maishani mwangu “mjasiri hawezi kuiacha asili” zilinijia ndani ya kichwa changu  kimawazo sikujari sana nilianza kutoka ndani ya kile chumba changu nikiwa na lengo la kwenda sehemu moja tulivu niliyo izowea siku zote kwa ajiri ya kupumzika na kuyabadirisha mawazo pamoja na fikra zangu.

Ndio ni mawazo yangu,na mengi ya mawazo hayo nilizoea kuwaza  kuhusu maisha,maisha ya kijijini,mawazo kuhusu kilimo chetu kitukufu  cha mahindi yatuleteayo  unga wa ugali,maharagwe yetu yatuleteayo mboga mboga ya majani ambayo kwetu tunaiita ‘’nguniani’’,karanga pamoja na alizeti zituleteazo  mafuta na masalia ya haya  maalizeti  yanatuletea mabaki mabaki  taka yake  tunayo yahita mashudu na hayo mashudu ni chakula kitamu sana kwa wanyama kama vile ngombe na mbuzi pamoja na ndege wetu kuku na bata.sio mazao hayo tu bali hapa kijijini kwetu mbozi tumejaliwa Baraka tele za mazao mbali mbali ya chakula na biashara.

Nilienderea kuwaza

Mawazo kuhusu nyuki watuleteao asali na sukari, mawazo kuhusu miti ya matunda matamu kama yale ya mabhohora,mapera,mafyurisi,makatapera au waswahili wayaitavyo  maparachichi,mahembe,mapeasi,ndizi sukari,mananasi,matunda damu na matunda mengine mengi sana.

Nilisongwa songwa na mawazo siku zote za maisha yangu ya kijijini,nikiamini kuwa jembe halimtupi mkulima,hapo ndipo nilijipa matumaini ya kufanya shughuri za kilimo na ufugaji kwa juhudi zangu kubwa mno.Ni ukweli usiopingika na usio pimika pale wazee wetu wa kijijini walipo tuhusia tusikidharau kilimo daima wazee wetu walitujaza elimu ya kilimo pamoja na ufugaji  wakatuambia  kwamba kilimo ndio utii wa mgongo kwa mwanadamu,asihelima na wala asipewe chakula kwani mdharau jembe si mkulima na huyo mdharau jembe nyumbani kwake hakuna chakula  kwa hali hiyo kilimo kwetu ni kazi moja  wapo tukufu kazi tunayo ienzi ili kujega  nchi ya kijamaa.

 

 

Tunalima viazi mbatata  pamoja na viazi mviringo,tunalima kunde,mbaazi pamoja na mtama,tuna mashamba ya miwa,migomba ya ndizi sukari pamoja na ndizi zile ziitwazo matoke,hatujapungukiwa kitu chochote kiitwacho chakula hapa kijijini kwetu mbozi na mkoa wetu wa mbeya,mkoa mashuhuri kwa wingi wa tani za chakula cha nyumbani na biashara.nilizoea sana kuwaza kuhusu kilimo pamoja na ufugaji wa wanyama kama vile mbuzi,ngombe,nguruwe,kondoo na mifugo mingine mingi tu ambayo mwenyezi mungu ametujalia.

 

Nilijikongoja kongoja taaratibu na kueleke mtoni,mkono wangu wa kulia nili likamata gitaa langu la nyuzi,gitaa nililolitengeneza mimi mwenyewe kwa ubunifu na kwa kipaji changu,japokua mimi sio mtaalamu wa masuala ya muziki ila niseme ukweli napenda sana muziki napenda kuimba kucheza na pia naweza kutunga nyimbo nzuri na tamu zinazohusu masuala ya mapenzi,siasa na za dini sanasana zile za kumsifu yesu kristo mkombozi wetu aliye tufia pale msalabani kwa sababu ya zambi zetu,makosa yetu na hatia zetu.

 Nilipo kua njiani natembea kwenda mtoni,taaratibu na kwa uangalifu mkubwa ili nisije kuchomwa na miiba au kungatwa na nyoka wa porini,kwani siku zote mimi pamoja na marafki zangu tumezoea kutembea peku peku popote pale tunapo kwenda, na jambo hili ni kama utamaduni wetu kwa sisi watu wa kijijini,moyoni mwangu nilikua najiimbia wimbo  ambao niliubuni kichwani mwangu muda ule ule nilio kua natembea kwenda kwenye kijito cha maji.

‘’ Zambi zetu pamoja na hatia,

Zambi zetu pamoja na makosa,

Mwenyezi mungu ametuhaidi,

Atatusamehe milele daima.

 

Ila tu iwapo tutamkufuru,

            Mwenyezi mungu hawezi kutusamehe,

             Imetupasa tusienderehe kutenda zambi,

Makosa ,hatia na kufuru,

Bali tumwombe mungu atusamehe.

 

 

Nikaenderea kuimba moyoni mwangu, huku nikitembea taaratibu;

                                           Utusamehe makosa yetu,

                                           Utusamehe zambi na hatia,

                                           Utusamehe bwana yesu   

                                           Utusamehe milele daima…….”

 

Nilifika mtoni mvua nayo ilienderea kutima,sikujari sana kama ningelowana au ningepatwa na homa kari kutokana na ubaridi wa mvua ile,sikujari hilo kwani  mimi na mvua ni mtu na rafiki yake,naipenda sana mvua,napenda maji yake matukufu yatokayo juu mbinguni,napenda sana kila niisikiapo ikilia juu ya  makuti na manyasi ya kijumba chetu,napenda sana kila nitizama mazao yetu yanavyo sitawi yanavyo mea na yanavyo kua kwa kasi kwa sababu ya uwepo wa mvua,natambua kua maji ni uhai pasipo maji binadamu hana uhai,pasipo maji mimea na wanyama wa kufugwa au wa mwituni au wa majini hawawezi kuishi .

 

Mvua kwangu ni rafiki yangu,ni mpenzi wangu na mwandani wangu,mimi na mvua ni chaunda chema kivikwacho pete,mimi na mvua hakika ni kidole na pete,tunapendana,na leo naiona mvua kubwa ya rasha rasha,inavuma pamoja na kusindikizwa kwa nguvu za upepo mkari,hilo siliogopi kwani najua kua mpenzi wangu mvua amekuja kwa faida yangu na pia kwa faida ya watu wote duniani pamoja na viumbe wengine wa porini au majini.niwe mkweli na muwazi ndugu zangu tusihizarau mvua mvua ni uhai wa dunia hii wapo ambao kwao mvua ni kitu nadra sana kupatikana,wapo ambao wanaishi kwenye majangwa ya kiu ya kukosa hata matone ya maji na maji yenyewe ni haya haya ya mvua,iweje sisi tuliobarikiwa  kwa uwepo wa mvua tunaidharau na kuona kuwa inatubugudhi.

 

Sikatai kusema kwamba aisifuye sana mvua inaweza ikamyea,ndio ni kweli kuwa mpenzi wangu mvua ana madhara yake mengi tu,japokua sina dhumuni lengo au haja ya kueleza madhara yatokanayo na uwepo wa mpenzi wangu mvua,lakini pia ni vema na itapendeza sana ikiwa sisi kama sisi tutajitahidi kuifadhi vyanzo vya mvua pamoja na kuyahifadhi maji yatokanayo na mvua ili yaje kutusaidia kwenye maisha yetu ya baadae kwani sisi binafsi hatujui yatakayojiri  baadaye mara tutakapo idharau mvua ni mwenyezi mungu pekee ajuaye yale mambo yote yaitwayo “future event”..

 

Mvua ilienderea kutima,ikanilowanisha mwili wangu wote ikalowanisha gitaa langu,nilijihisi kama vile nabarikiwa  kwa kubatizwa mar azote  niwapo katikati ya maji ya mvua,macho yangu yalilowana,nguo zangu zililowana tipwa tipw,nywere zangu ndefu zililowana shagharabagha,gitaa langu bado lilikua lipo “stable”linanguvu ya kuimiri yale mawe mawe yatokayo juu kwa sababu ya barafu ya mvua.taaratibu nilizigusa nyuzi za gitaa langu na taaratibu nilianza kulikunguta,kulicharaza na kuliponda ponda gitaa langu kwa vidole vyangu virefu katika mikono yangu.

 

Mvua ilienderea,ikaenderea na kuenderea bila kukomaa na mimi kadri mvua ilivyozidi kuninyea nilipandwa na hisia kari sana mara baada ya kuanza kuimba wimbo wangu mtamu niupendao kila siku,na wimbo niuimbao usiku na mchana,pasipo kuchoka;

Kwenye kijito cha maji,hapo naoga,

Maji safi yatokayo,yatokayo mbinguni,

Kwenye kijito cha maji,kuna damu ya yesu

Imenisafisha zambi,imeniponya magonjwa.

 

Kwenye kijito cha maji,njoni ndugu zangu,

Njoni tuhogerehe,maji safi yatokayo,

Yatokayo mbinguni,kuna damu yesu

Atatusafisha zambi atatuponya magonjwa….

 

Hisia zangu zikanivuta nienderehe kuimba ,nami kwa vile nimejariwa kipaji cha kumwimbia na kumsifu mwenyezi mungu nikaughani wimbo mwingine.

Nataka,nataka,nataka,nataka,nataka

Nataka kumjua mungu,nataka nataka

Nataka kumjua mungu,nataka,nataka,

Nataka kujua mapendo yake,nataka,nataka,

Nataka kujua rehema zake,nataka,nataka

Nataka kujua nehema zake nataka nataka

 

 

Nataka nataka,nataka,nataka,nataka,nataka

Nataka,nataka,nataka,nataka,nataka,nataka

Amenipenda bwana,nataka,nataka,

Amenivuta kwake,nataka,nataka nataka

Ameniita yesu,nataka nataka

 

Na kadri nilivyo zidi kuimba wimbo wangu ule mtamu,hisia zangu zilizidi kupanda na sauti yangu ilipanda na kushuka ,ilipanda kwenda juu mbinguni,ikashuka kuja duniani na nina uhakika mkubwa kwamba watu wengi sana katika kijiji chetu walisikia jinsi nilivyo kua naimba,kwani ni kawaida yangu kuimba kwa sauti ambayo wanakijiji huisikia vema,na mara nyingi hawasiti kunisifu au kunipongeza kwa sababu ya kua na sauti tamu sauti nzuri ya kuwatoa nyoka, mapangoni.

 

Mara baada ya kuimba ule wimbo wngu kwa kurudia rudia  mara nyingi zaidi,nilishusha pumzi zngu ndefu nikapepesa pepesa macho yangu  huku na uko kushoto na kuria katika kijito kile name nikaona  jiwe moja kubwa la chuma lipo hapo upande wa kuume kisha nikajivuta jivuta  taaratibu kwa kujilazimisha mfano wa kinyonga anae tembea na baada ya  kufika kunako ilo jiwe nilijikarisha kimatanga nikiwa nakitamani kughani wimbo mwingine ndani ya moyo wangu.

 

Ghafra mvua ika stop kuenderea kutima na kustop  kule kulikua ni kama  tukio la ghafra mno  tukio lililonifumbua mdomo wangu na kunifanya nipigwe na mshangao kwani sikujielewa elewa kwa nini nipo katika hali ile,hali ya kunishangaza na kunigeuza bumbuwazi.mwili wangu ulikua umekauka kau kama vile  nilipigwa na jua la saa sita kwa muda mrefu,nguo zangu nazo zilikua zimekaukaa na kuwa kama vile zilianikwa kwenye jua kwa muda mrefu,sio nguo na mwili wangu tu,bali hata gitaa langu nalo lilikua limekaukaa kau acilia mbali neo ambalo nilikuwepo hapo mwanzo lilijaa matope matope pamoja na mrundiko wa maji machafu lakini sasa lilikua ni eneo ambalo limekauka limeota nyasi na kutoa maua maua,nilijisha ngaa na nilishangaa eneo lile,sikuelewa na wala sikujielewa elewa nilibaki kujiuliza kwa sekunde kaza nini kimetokea?kuna nini ?je naota au ni kweli?mbona sielewi.

Nikiwa bado nimepigwa na butwaa nilisikia mlio wa sauti kubwa pamoja na miungurumo ya radi kari,radi ambayo hakika katika maisha yangu sijawahi pata kuisikia ,kwani ilikua ni radi moja yenye mlio mkari sana,mlio ambao hakika wewe ndugu msomaji kama ungepata kuisikia ilke sauti ndani ya sekun de chache ungekua uhu  marehemu safari yako ya kwenda kumwona bwana yesu juu mbinguni ingekua karibu kutimia,lakini namshukuru mungu nipo hai sikuona madhara yoyote ya pasuko la ile radi.

 

Nikiwa bado naenderea kupigwa na butwaa mahari pale kwenye kijito cha maji nilikuja kuisikia  sauti moja ya mwanamke,ikininongoneza kunako masikio yangu  na kunongoneza huko kulikua ni kwa  taaratibu.nikasikia sauti ya mwanamke huyu ,mwanamke mtu mzima ikiniambia;

                  “Tizama juu”

Nami nikaitii ile sauti,sauti laini na nyororo,,nikatizama juu ilikuona ni nini ambacho napaswa kukiona

Sikuona kitu zaidi ya mawingu mawingu yale yaliyo jikusanya kuanza kujikunjua kunjua na kuacha  anga la bluu.ndipo nikayashusha macho yangu chini ya aridhi

Moyo wangu ukaniulza tena

 “je umeona nini”.

Name nikaujibu moyo wangu kwa heshima zangu zote na taadhima

“nimeona mawingu mawingu meupe yakijitawanya tawanya na kuliacha anga la buluu”

 

Kisha moyo wangu ukaenderea kusema.

“ Umejibu vema Tizama tena anga la juu”

Mvua ilikoma kwa muda ule,muda ambao binafsi niliona kama ni miujiza  au mauza uza  flani fulani,yakitendeka mahari pale nilipokua nimesimama bado sikuelewa nini maana ya mabadiriko yale, nikajisemea kimoyo moyo au je ninaota, na je ninaota ndoto za mchana, la hasha!! Moyo wangu ukanijibu,hauoti ndoto za mchana ni kweli haya yote unayoyashuudia yana tokea.

 

Nikatizama tena juu ya anga la dunia.

hapo ndipo woga hofu na kutetemeka kukanivamia sana,tetemeko langu lilikua ni kama vile napigwa na nguvu furani za umeme,nguvu ambazo ziliinyonya damu yangu yote na kunikausha mwili wangu wote na mwili huo nilihisi umekauka kama mfano wa gogo au mti mmoja mgumu uliokaushwa na jua.niliogopa nikatamani kukimbia,nilihofu almanusura haja zangu zote kubwa na ndogo zinitokee kwa pamoja,niliogopa kwa sababu ilikua ni mara yangu ya kwanza kukumbana na hali ile.

Nikauinua mguu wangu wa kushoto lakini mguu huo haukuweza kuamka,nikauinua mguu wangu wa kulia vivyo hivyo mguu wangu wa kulia nao haukutaka kusimama,mpango wangu wa kukimbia ulishindikana,nikajiona kama nipo katikati ya kifo nipo njia panda wala sijui ni wapi pa kukimbilia.

 

Juu ya lile anga la ubuluu  ubuluu wa rangi iliyokorea alisimama mwanamke,mtu mzima wa makamo,mnene na unene wake ni unene wa mtu mzima,mrefu ameachia tabasmu mdomoni mwake,na tabasamu ilo halimtoki kwa muda wote tangu namtia machoni pangu,ni wa rangi ya chungwa lililoivaa haswa au waswahili wa kisasa wao wanaita ngozi ya kizungu,nywere zake ndefu nyeusi tii zenye mg’aro kichwani mwake.amevaa mavazi meupe na weupe wake ni weupe ajabu hakuna mavazi kama yale duniani popote,nilienderea kumtizama huku nikiwa na hofu kuu ya kumwona kiumbe Yule juu ya anga la dunia,niliogopa kwani ile ilikua ni mara yangu ya kwanza kushuhudia kiumbe kile kikiwa juu ya anga la dunia,kwangu mimi ilikua ni zaidi ya maajabu au miujiza kwani kwa hisia zingine nilihisi labda kiumbe Yule ni roho mwovu aliye tumwa kuja kunidhuru,haikua hivyo nilikua katika hali ya kuandikia mate wino ungalipo,kwani nisilolijua litanisumbua na nisilolifahamu ni kama usiku mnene wa manane.

 

Nilienderea kumtizama mwanamke Yule naye alienderea kunitizama,macho yake yenye mboni zenye ubuluu yalizidi kupendeza usoni mwake,lakini kupendeza huko kwangu mimi kulinitisha kwani sikuwahi kumwona  mwanadamu mwenye macho ya rangi ile ya kibuluu,nimezoea kuwaona watu wenye macho yenye mboni nyeusi,nyekundu au ile ya kaki lakini macho haya ya rangi ya kibuluu yalinitisha sana niliogopa hakika niliogopa na kuhisi kuwa nipo hatarini.

 

Sikua na nguvu tena za kukimbia au kumkwepa mwanamke Yule,kwani miguu yangu haikuweza kufanya jambo lolote lile sembuse iwe kukimbia,kutoroka au kumkwepa mwanamke Yule.nilienderea kumchunguza ,kwani umbali aliokuwepo yeye ni umbali ambao macho yangu yaliweza kumwona,yaani hakua mbali sana na upeo wa macho yangu,ilikua ni kama mbingu alizokuwepo yeye zilikaribiana na dunia hivyo basi shida ya kumwona haikuwepo kabisa ,alinitizama na mimi nilimtizama,aliniangalia na mimi nilimwangalia,tulienderea kutizamana.

Mikononi mwake alishika kitu kama kitabu chenye rangi ya dhaabu safi kunako jarida lake,nilikitizama kile ktabu na baada ya kukitizama niligundua kua ni biblia takatifu,ameikamata mkono wa kulia kwake,mkono wake wa kushoto hakua na kitu chochote  mkono huo ulikua mtupu.nikamtizama tena katika pembe za mabega na mgongo wake  alikua na mabawa makubwa sana ,yalikua ni makubwa kuliko hata ndege wa angani,yalikua makubwa yenye  manyoya marefu yameambatana pamoja na kushikana na mifupa ya  mbawa zake.

 

Tuliendelea kutizamana kwa sekunde chache mbeleni.

Kisha nikamwona anapaa kwa mbawa zake anashuka chini kutoka kwenye lile anga la dunia hofu na woga vilizidi kunitawala nilijua labda anakuja kunidhuru nafsi yangu,lakini hapana moyo wangu ulinikataza kuamini hivyo kwani macho yangu yalipotua kwenye mikono yake na kumwona amekumbatia biblia takatifu nilijua kiumbe huyu hana madhara yoyote kwangu,amekuja kwa nia njema na pia amekuja lengo au dhumuni fulani.

 

Akashuka taratibu hata akanifikia pale nilipo simama  na baada ya kunifikia yale mabawa yake yakapotea kwa ghafra,lile vazi lake jeupe likapotea kwa ghafra na ile asili yake ya kizungu ikampotea kwa ghafra sasa akawa ni mwenye rangi ya mkaa au ile rangi ya chungu kilichopigwa sana na nguvu za moto wenye kuni nyingi, rangi nyeusi rangi ya kiafrika,mwili wake ulikua vile vile,labda niseme macho yake yale ya kibuluu nayo yakabadirika yakawa yana mboni ya rangi nyeusi,urefu wake ulikua vile vile,unene wake nao pia ulikua vile vile.

Sasa alionekana amevaa gauni lenye rangi rangi mchanganyiko rangi zilizo kolezwa na kupambizwa madalizo ya maua maua mazuri ajabu,maua ambayo sijapata kuyaona duniani hataleo hii sitakuja kupata kuyaon.

 

Mara baada yay eye kushuka chini ya aridhi kutoka katika anga la dunia,nguvu za miguu yangu zilinijia,niliweza kutembea kama nilivyozoea,ile hofu woga na tatiziko la moyo wangu vikapotea na sasa sikuweza kuogopa au kutatizika tena,hali hii ilinishangaza mimi binafsi kwani ni kitambo tu niyaone mabadiriko haya yakinitokea,kwani mwanzo nilikua na tetemeko,hofu na woga,lakini ajabu ni kwamba sasa nina amani furaha na tumaini.

 

Nilijiuliza mara mbili mbili mimi ma moyo wangu,nini ni haswa maana ya kutokewa kwa hali kama hii,lakini moyo wangu haukuwza kunijibu kinagaubaga zaidi ya kuwa na subira kwa kadri ya nuckta,dakika na masaa yatakavyo kwenda mbele.

Tulitizamana tukiwa wote tumesimama sentimita chache mbele yetu,tabasamu lake pana halikumtoka mdomoni kwani meno yake meupe yaso na mfano yalimpendezesha zaidi na kumfanya awe mzuri zaidi,mara baada yayeye kutabasamu name pia nilitabasamu,tukatizamana,akatembea kunijia mahari nilipokua nimesimama pale pale kwenye jiwe kubwa la chuma,pale nilipoweka gitaa langu nilililotumia kuitumbuizia nafsi yangu dakika chache zilizo pitaa.akatembea mwanamke Yule,akatembea mpaka nilipokua nimesimama,nikamwona anaunyosha ule mkono wake wa kulia   mkono alioikamata biblia takatifu akaielekeza kwenye mkono wangu wa kulia,kama ishara ya kunipa ile biblia takatifu.

 

Name sikusita,nikainyosha mikono yangu yote miwili ili kuipokea ile biblia takatifu,sijui niliupata wapi ule ujasiri wa kupokea ile biblia,na baada ya kupokea ile biblia akanitizama kwa macho yake yote mawili kisha akatabasamu,tabasamu lile lile zuri lenye utajiri wa hekima,busara,wema pamoja na  mambo mema  yenye neema na yenye rehema.na baada ya kuipokea ile biblia taktifu  mwanamke yule akanipita pembeni yangu nikamwona anaelekea  eneo ambalo  kijito kile kilikua kinayapeleka maji kwenye mkondo wake.

 

Nilienderea kumsindikiza kwa macho yangu yote mawili ili nione ni wapi anaelekea nan i wapi mwisho wa safari yake,hatua kwa hatua nilimsindikiza kwa macho yangu yote mawili hata alipofika kwenye   ule mto nilimwona akiinama chini kwa mtindo wa kuchuchumaa,na baada yay eye kuchuchumaa nilimwona akiokota kopo kubwa la platik kisha akautwaa na mtungi ambao mpaka leo hii najiuliza maswali ni wapi aliupata  ule mtungi na lile kopo kubwa la plastick kwa sababu mtoni pale hapakuwa na kitu chochote cha kutekea maji zaidi ya maji yenyewe yalivyo kua yakisafiri kwa mwendo wa kujisukuma chini chini pamoja na mchanga mwingi ulio kuwepo pale mtoni kama vile mchanga wa baharini.

 

Na alipokwisha kutwaa lile kopo la kutekea maji pamoja na ule mtungi,mwanamke Yule akaanza kuyachota yale maji safi ya mtoni na kuyaweka kwenye ule mtungi,alifanya hivyo kwa kurudia rudia  mpaka pale aliporidhika yeye mwenyewe kwamba ametosheka na kiasi cha maji ambayo alikua anayateka.

Nilimtizama tena nikamwona anafungasha ngata kwa kutumia kitenge chake kizuri alichojivika kiunoni,na bada ya kufungasha ngata  malaika Yule akauinua mtungi wake wenye maji yaliyo pwaa hadi juu ya mdomo wa ule mtungi kisha akajitwika kichwani  pake.tendo lote lile alilokua akilitenda mwanzo mpaka hatua ya mwisho ya utekaji way ale maji mimi nilisimama  mahari pale pale aliponipita nikimtizama  kwa kila tendo alilokua akilitenda.

Alipojitwika ule mtungi wa maji mwanamke Yule akakanyaga hatua moja kutoka kwenye  pembe ya kile kijito cha maji nikamwona anainua mguu wake ili aondoke mahari pale lakini ghafra ule udongo ulioshikilia kile kijito cha maji ukamengenyuka  mengenyuka na baada ya kumengenyuka udongo ule ulididimia chini na kuingia kwenye  mto ule yaani kwa kifupi ilikua ni kama mmongonyoko mdogo wa udongo .mmongonyoko ule ulitokea kwa ghafra sana  hali ambayo  hakuna aliye itarajia si mimi wala si mwanamke  Yule.

Kitendo cha kumongonyoka kwa ule udongo kuliperekea mwanamke Yule ambaye muda mfupi tu alipotua chini kutoka juu ya anga la dunia nilipoteza kumbukumbu za kumtambua yeye kama malaika name nikamwona kama binadamu  wa kawaida kama binadamu wengine walivyo, ujio wa  mwanamke huyu lilika ni kama tukio la ajabu sana katika maisha yangu binafsi kwani mbali nay eye kuja kama malaika alijibadirisha ule mwili wa kiroho na kuwa binadamu wa kawaida  akaichukua nafsi yangu ya kumbukumbu  na kuipoteza kimiujiza hata sikuweza kukumbuka wala kutambua kuwa nipo na roho wa kimungu ambaye amejibadiri na kuwa roho wa kibinadamu.

 

Nilishuhudia mmongonyoko ule wa udongo ukimwangusha chini ya aridhi na kumsukumia  mwanamke Yule,akaanguka na kudondokea kwenye  mto kitendo cha yeye kuanguka na kudondokea ndani ya maji ya ule mto kilimfaanya apige ukulele wa kuomba msaada,akitapatapa na kuvutwa na maji mengi ya ule mto,akitapatapa na kusukumizwa  mbali sana na  ule mto.niliogopa nilipo ona tukio kama lile likitendeka tena mbele ya macho yangu,niliogopa na niliingiwa na hofu kuu kumwona mwanamke Yule akigugumia  vikombe vya maji yale ya mtoni.

 Maji ya ule mto yalienderea kumvuta na kumsukumizia mbele ambako mto ulikua unayapeleka maji yake,yalikua yakimvuta kwa mwendo wa kasi sana,yalikua yakimvuta kama vile mafuriko ya mvua yanavyo vuta takataka au kitu chochote kile kinachoweza kubebwa na maji nilishuhudia namna anavyo zama na kuibuka akipiga kelele za kuomba msahada .

 

Haraka sana kengere ya hatari ikaria ndani ya ubongo wangu,ikaniambia nifanye jambo la ziada ili kuyaokoa maisha ya mwanamke  Yule,nikazipiga  mbio mpaka  usawa wa ule mto na kisha nikajitoma mpaka ndani ya maji ya ule mto nikazama na kuibuka ……nikazama na kuibuka….nikazama na kuibuka  nikimtafuta mwanamke Yule ambaye baadaye sana niligundua jina lake anaitwa magdallena,nikazama tena sikumwona nikaibuka tena sikumwona nikajua sasa hapa kuna hatari kubwa  ndani yam to ule, kwa vile nilikua na ujuzi wa kucheza na maji sikupata shida sana kuzama na kuibuka kwani staili hizi mbili ni staili nilizozizoea sana mara ninapokuja kuogerea katika mto huu.

No comments:

Post a Comment