Thursday, November 26, 2015

                               KISWAHILI  YETU  MALI.

1. Asante sana Kaimu, kwa wingi wa ukarimu,
Nimesimama Sekomu, Na kuandika kalamu,
Maneno yangu matamu, kuyasikia wazimu
Nimekuja, na ujumbe Kiswahili yetu mali.

2. Kiswahili ni Asali, kukitamka fahari,
Kiswahili kwangu mali, faida yenye johari,
Mimi mwenyewe nakiri, utamu wake sukari,
Na tafakari fikiri, hakina mwisho bahari.

3. Katika dunia leo, twalia maendeleo,
Twatamani vingi vyeo, vilojaa upendeleo,
Vitamu tamu vyeo, twataka mafanikio,
Lakini na ipo siri, tutumie Kiswahili.

4. Ukitaka pata elimu, ukitaka pata ajira,
Jambo moja la muhimu, na ndio ngao na dira,
Nimuhimu kufahamu, kwa hekima na busara
Kiswahili ni kitamu, utamu wake sukari.

5. Kiswahili kwetu mali, utajiri wa dunia,
Utamaduni asili, lulu yetu watanzania,
Baraka za kila heri, mataifa yalilia,
Kiswahilli lulu yetu, Ni mama waki Afrika.

6. Tupo juu Tanzania, sababu ya Kiswahili,
Sisi tunajivunia, umoja wetu wa kweli,
Amani yetu dunia, sababu ya Kiswahili,
Tukilinde Kiswahili, tukitunze Kiswahili.

7. Tusijeona aibu, kukisifu Kiswahili,
Huo Ndio wetu  wajibu,ngao  tunaikubali
Yenye faida zahabu, lugha yetu Kiswahili,
Mwende kwao si mtoro, cheza kwenu utatunzwa.

8. Tuoneshe uzalendo, kutetea Kiswahili,
Na tufanye kwa vitendo, kutangaza Kiswahili,
Pasiwepo hata nyondo, kukipelekea mbali,
Huo Ndio  ujasiri, kujaipenda asili.

9. Mungu asiye achuki, karama zake kufanya,
Africa ya mashariki, lugha bora imepenya,
Mazuri mengi lukuki, keswahili kimeshafanya,
Tuna haja kukienzi, na tunzo kukipatia.

10. Tukitangaze Arabu, kemejaa maajabu,
Na wasione aibu, lugha hiyo mahababu,
Watamke bila tabu, lugha hiyo ya mababu,
Hakika wanatamani, mali yetu ya thamani.

11. Tusiweze kukitupa, maana kinatulipa,
Furaha na kunenepa, tukipita twajitapa,
Kwa wingi kimetulipa, wingi wake wa nafaka,
Nehema nayo rehema, fadhili nazo heshima.

12. Tunahaja kukienzi, na tuzo kukipatia,
Kimekwisha jaa mapenzi, na dua  ku kiombea,
Kwa mashairi na tenzi, nyimbo bora kusifia,
Kiswahili barikiwa, malaika wakwambia.

13. Kiswahili barikiwa, malaika wakwambia,
Marefu maisha jawa, dua njema twakuombea,
Kiswahili barikiwa, malaika wakwambia,
Marefu maishajiwa, malaika wakwambia,

14.  Ewe  Mama nenepa, wajibu ni kukutunza,
Afya ni supa supa, kula mama unaweza,
Mimi mwenyewe naapa,mama yangu kukutunza
Mbele sana utafika usiwe nayo mashaka.

15. Wengine ni mabatili, ni bora wakajinyonga,
Hawasomeki fasili, wahangaika  kulinga,
Waondoke majangili, mwendo wao wa vinyonga,
Wakupishe mwana mwali, uitawale dunia.

16. Yamewafika shingoni, wamebaki tapatapa,
Nyota zao zi gizani, hata mwanga watopata,
Ewe jua dunia, uwachome fasta fasta,
Wafuta kwenye ramani, wasahaulike dunia.

17. Kipichakung’ang’ania, hatuwataki timua,
Kwanza wamesha chelewa, wataishia kunawa,
Muda watupotezea, waende wakanye jera,
Hiyo mali  mkoloni, haina thaamni mama.

18. Wanaitwa kingereza, wengine ni kifaransa,
Mama hao wameoza, yatupasa kuwasusa,
Wananuka mafunza, ni bora kuwanyanyasa,
Waarudi ughaibuni, hatuwataki hasirani.

19. Hao ndio mashangingi, tena wanavuta bangi,
Wapepesuka mitungi, za fifia zao rangi,
Ndio waeneza gonjwa, tumewapima angaza,
Wamelazwa kwa vitanda, wayaona majeneza

20.  Niseme  kwa kinyakyusa, kibantu nakitukuza,
Kuliko sema faransa, lugha nisiyoiweza,
Napata faida gani, kutukuza kingereza,
Napata faida gani kutukuza kingereza

21. Moyoni ninawacheka, watumwa maghaaribi,
Wamemezwa wametekwa, mawazo ya kumbikumbi,
Hakikia wanateseka, jamani uongo  zambi,
Kiwahili wakomboe, kiswahili waokoe.

22. Nipo hapa kuwachamba,waache jigagamba,
Kwanza hao ni washamba,shuleni hawajatimba,
Hapa mama watalemba, na kuimba wataimba,
Kiswahili wetu simba,uitawale dunia.

23. Wazee walao  chumvi, vijana wapeni hekima
Siyakimbie majamvi, yasofaidisha vema,
Yamejaa maugomvi, malipo yake  vilema,
Kama kawa kama dawa, kitukuzwe Kiswahili.

24. Siku njema asubuhi, dua kuku mpate mwewe, 
Pole pole tutawahi,Tusikipate kiwewe,
Mwenyezi si athumani, alo juu mngoje chini
 Mpanda ngazi tashuka, Kiswahili tatawala

25. Tujipe matumaini, na pia tujiamini,
Mioyo yenye amani, tufe nayo kikondoo,
Beti  ishirini na sita, mkono nimeimba fasta,
Masikini mi jamni, natamani kwendelea.

26. Tamati nimefikia, natamani kwendelea,
Giza  limesha ingia, kalamu yanigomea,
Mimi naitwa Elia, Mwalukali wa kumbeya,
 Mwenyezi mungu  jalia, kesho tuonane pia.

No comments:

Post a Comment