Monday, November 30, 2015

KAZI TUUUUUU




By Joster Mwangulumbi
Sitaki umbea wala kuumbua watu. Miaka yote zikifanyika sherehe za Uhuru na nyinginezo, wasomi, wanasiasa na wananchi wa kawaida wamekuwa wakisifu maandalizi yake na kwamba zimefana. Hawakosoi.

Leo watu haohao wanamsifu Rais John Magufuli kwa kufuta baadhi ya sherehe hizo. Magazeti yanasifia tu. Fungua gazeti lolote huwezi kukosa vichwa: “Kasi ya Magufuli yatanda kila kona;” “Magufuli usipime;” “Magufuli atisha;” “Magufuli…” Hivi amefanya nini kipya, kufuta safari za nje? Je, amefuta safari au hali ya fedha inamlazimisha aangalie maeneo fulani ya kipaumbele?

Mtangulizi wake, Jakaya Kikwete alikuwa anajisifu, Magufuli anatenda ili wengine wamsifu. Ndiyo maana mara anatangaza kufuta ziara na sherehe, mara kavamia Hazina, Muhimbili, mara mikutano serikalini kufanyika kwa video, mara hakuna kuchapisha kadi kwa fedha za Serikali, mara amewamwaga vigogo TRA. Kesho yake magazeti yanampamba na kumjenga.

Ole wao watangulizi wake wadai kwamba anawaumbua! Ole wao CCM walalamikie kasi yake! Magufuli anajua watakaomnyoshea kidole watakumbana na nguvu ya umma.

Magufuli anajua alipata upinzani mkali wakati wa kampeni kwa sababu wapinzani kwa muda mrefu walijijenga kwa wananchi kwa kaulimbiu ya nguvu ya umma.

Katikati ya kampeni aliiga mbinu za wapinzani na hata kukarabati sera za CCM kuvunja zilizokuwa zinanadiwa na wapinzani. Sasa anatekeleza.

Hebu tazama suala la sherehe. Wapinzani walipojinadi mwaka 2010 na mwaka huu wakiingia madarakani watafuta baadhi ya safari za nje na sherehe halafu watauweka Mwenge wa Uhuru katika makumbusho ya Taifa, Rais mstaafu Benjamin Mkapa aliwashambulia kwa maneno makali. Hata wasomi wenye mrengo wa CCM waliwaona wapinzani watu wa ajabu sana.

Leo wasomi walewale waliokosoa mkakati wa wapinzani (CUF, Chadema, NCCR - Mageuzi) wa kufuta sherehe za kitaifa, ndiyo wanaompongeza Magufuli kwa anachokifanya. Sipati picha Mkapa anajisikiaje anapoona “mtoto wao mpendwa” anatekeleza sera aliyoilaani.

Kasi ya Magufuli imesababisha wasaidizi wa wilayani wanaumiza watu. Novemba mwaka jana akiwa Kamanda wa Uhamasishaji wa UVCCM, Paul Makonda anadaiwa ‘kumlamba za uso’ aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji mstaafu, Joseph Warioba. Waliolaani utovu ule wa nidhamu ni wapinzani na wanaharakati tu.Mapema mwaka huu akateuliwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni. Wiki hii akatangaza kuwasweka mahabusu kwa saa sita maofisa ardhi 20 wa manispaa hiyo kwa kuchelewa kuwasili katika ziara ya kutatua migogoro ya ardhi katika manispaa hiyo.

“Hii haikubaliki hata kidogo. Mimi niliwasili kwa wakati, Ofisa Tawala wa Wilaya (Das) aliwasili kwa wakati na hata Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni aliwasili kwa wakati. “Tulilazimika kuwasubiri (maofisa ardhi) kwa saa tatu nzima hadi saa tano asubuhi kwa sababu bila wao hakuna kitu ambacho kingefanyika,” alisema.

Makonda alidai baada ya kubaini muda uliosalia usingetosha kufanya ziara hiyo, alilazimika kuiahirisha na kuamuru kukamatwa maofisa hao kwa kile alichodai kosa la dharau na kukosa heshima kwake akiwa kiongozi. Alisema uamuzi huo aliufanya ndani ya sheria kama Mwenyekiti wa baraza la ulinzi na usalama la wilaya hiyo.

Hivi kitendo cha Makonda kutangaza ‘kulostisha’ maofisa ardhi kwa saa sita mahabusu kwa kuchelewa ndiyo njia ya kuchochea kasi ya uimarishaji utumishi wa umma au ndiyo utekelezaji wa kaulimbiu ya “Hapa Kazi Tu ya Magufuli?” Je, Makonda ni mamlaka ya nidhamu?

Baadhi wamefurahia hatua hiyo, lakini nadhani Magufuli hatafurahi kiongozi kutumia vibaya madaraka. Kama ni mchapakazi kwa nini hali imefikia hapo? Si anastahili kuadhibiwa kama Kikwete alivyofanya.

Februari 2009, aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Bukoba, Albert Mnali aliamuru walimu 32 wachapwe viboko kwa madai walisababisha wanafunzi kufeli katika shule za msingi zilizoko Bukoba Vijijini. Alifukuzwa kazi; siku hizi ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nachingwea. Aprili 2010, Sungusungu wa Shinyanga wakaamua kuwacharaza bakora walimu wanne akiwamo mwalimu mmoja mwanamke ambaye alikuwa ni mjamzito kwa kosa la kuchelewa kwenye kikao cha walimu na wazazi. Sungusungu hao nao walishughulikiwa. Vipi Makonda?

Haya Polisi wa Mwanza, wanahangaika kuzuia kuagwa maiti. Wameacha kazi ya kulinda amani na usalama wanazuia watu wasikusanyike kuaga maiti ya mpendwa wao aliyeuawa kwa kuchinjwa na watu wanaodaiwa kuwa makada wa CCM. Mwanasheria wa Serikali anajitokeza kudai eti marehemu Alphonce Mawazo asiagwe Mwanza kwa vile si kwao. Kweli Serikali inathubutu kutoa madai ya kibaguzi kama haya? Wanaodhani wanamridhisha Magufuli wataumbuka. Tusubiri.

WORK NOTHING ELSE....HAPA KAZI TU




He’s been office for all of three weeks and already Magufuli has earned a reputation for rocking the boat, with his no-bullshit attitude and corruption-busting plan of action.







Sure he’s the son of a farmer, but this guy’s far from simple; his first real job was a school teacher, thereafter he educated himself as an industrial chemist and eventually became Tanzania’s minister of public works. The latter position saw Magufuli tackle some of the country’s largest construction projects without even a whisper of corruption or maladministration. In fact, he’s well-known for being a-corrupt, seriously.



So what is it that makes John Magufuli so great? Well, unlike so many of his counterparts, he’s relentless in his assault on corruption, laziness, and overspending; something that no doubt has already made him very unpopular among his own political comrades as well as leaders like Zuma and Mugabe. Let’s face it; the man makes almost every other leader look like a thief.



Three weeks in office and we’ve already got at least 10 major changes to report, imagine what the man can get done in five years.



Have a look at some of this legend’s highlights so far:



He cancelled Independence Day celebrations, saying that it’s “shameful” to celebrate while people are dying of cholera. Instead, the money that would have been used has now been set aside for street and public area cleaning.



After visiting the Muhimbili Hospital for the first time and seeing the dire state of affairs, the president ordered that more than 200 million Shillings earmarked for parliamentary parties be used to upgrade the hospital facilities. Less than a week later the hospital had 300 extra beds. He then fired the entire hospital board and had broken equipment repaired.



Magufuli cut his inauguration party budget from $100 000 to just $7 000 and gave the difference to the very same hospital mentioned above.



In his first week he ordered a ban on all international travel by government officials; adding that they need to focus on the rural areas of Tanzania and the poor, while commissioners and ambassadors who are already overseas can fulfil any foreign obligations.



All first and business class flights are off limits for government officials; except the president, vice president and prime minister.



Government workshops will no longer be held at hotels and function halls. Instead, they will be held at government-owned chambers so as to use what has already been paid for.



He fired Tanzania’s chief of revenue after 350 containers listed in his books disappeared from Dar es Salaam harbour. The prime minister is currently heading up that investigation.



He appointed the country’s very first female vice president.



When he had to travel 600km from Dar to Dodoma to open parliament; he chose to drive himself rather than have government organise a jet.



Magufuli went on record in the national assembly saying that, now that he’s president “it will not be business as usual.”



Pretty f*cking cool right? Well, here’s one more thing you might like to know about “The Bulldozer;” yeah, that’s what they’re calling him.



His tagline for his presidential campaign was “Work, nothing else.”

FIND ME IN AFRICA

FIND ME PLEASE
eliaabelia25@gmail.com
Face book name;Elaija Elia
Instagra;Elaija Elia
phone;(255)655496518
or.......(255)654614557

ABOUNDATS LOVE....LOVE THAT ALWAYS SPEAK















AWESOME...SOME TIME













YUO MUST SAY AFRIC IS BEAUTIFUL









nNEWS....NEWS...TODAY NEWS

CAN YOU BELIEVE WHAT TANZANIA's NEWLY ELECTED PRESIDENT MAGUFULI IS UP TO ??

UPDATES FROM TANZANIA POST ELECTION ACTIVITIES

Last weekend they were opening parli...ament and there was a state dinner planned for all guests that was going to cost about 300m. President Magufuli cut the budget to 25m and ordered that the rest be taken to buy hospital beds for Muhimbili they got 300 beds and mattresses and 600 bed sheets from that money.
On 23rd Nov 2015 he announced that there will be no official ceremonies for Independence Day on 9th December, the money is to be used for more pressing issues and the day should instead be spent cleaning up our environment.
On Saturday 21st nov 2015 a group of 50 people were about to set off for a tour of commonwealth countries (don’t know for what) but President Magulufi cut that list down to 4 people, saving government 600m in tickets, accommodation and per diems
No more foreign travel, embassies will take care; if it’s necessary to go, special permission must be sought from him or Chief Secretary
No more 1st class and business class travel for all officials except President, Vice, and Prime Minister.
No more workshops and seminars in expensive hotels when their so many ministry board rooms available.
President Magulufi asked how come engineers are given V8s when a pick-up is more suitable for their jobs.
No more sitting allowances, how the hell are you paid allowance for a job which you have a monthly salary; that also applies to MP’s.
President Magulufi has literally pressed the reset button; returning Tanzania to default factory settings, because that was the TZ Nyerere left us with.
On the day after he was brought to power, in the morning as State House officials were showing him round he decided to take a walk to ministry of finance, told them to get their act together, asked why some employees weren’t in office (ever since then the traffic jam in mornings has become worse) and ordered TRA to scrap all tax exemptions, everyone must pay taxes especially the big guys
President Magulufi went to Muhimbili Hospital unannounced and walked thru the worst parts that they keep hiding from important visitors he fired the director, fired the hospital board and ordered that all machines that weren’t working (so that people go to private hospitals owned by some doctors) to be repaired within 2 weeks otherwise he fires even the new director; the machines were repaired in 3 days
Finally, last week when going to officially open parliament President Magulufi didn’t go by plane, drove the whole 600km from Dar to Dodoma.
President Magulufi has reduced the size of the presidential convoy, even reduced the size of presidential delegation that travels with him
President Magulufi chose a Prime Minister we haven’t heard of before, a guy with reputation for hard work and no corruption all the big guys we expected could be PM have been let wondering what hit them.
His motto is: Hapa Kazi Tu = "HERE, ALL WE DO IS WORK/ SERVE!"
After President Magulufi visited Ministry of finance and Muhimbii Hospital without announcing it is said the port (most corrupt, delaying, thieving officials) were all of a sudden the most efficient place. No loads are missing, things are done quickly and that habit of forcing for a bribe so that your container is released is no more.
Oh, they say when he was confirmed as winner people started congratulating him and wanting to bring gifts to his place he turned them back, saying he will receive all congrats over the phone, nobody should visit him.
All individuals/firms that bought state companies that were privatized but haven’t done anything (20yrs later) are to either revive the industries immediately or hand them back to the government

 
VIPAUMBELE VYA RAIS MAGUFULI
1.Mapambano dhidi ya Rushwa na ufisadi(kuanzisha Mahakama ya Rushwa/Wahujumu uchumi).
2. Utatuzi migogoro ya ardhi.
3. Kuimarisha Bandari.
4.Ukosefu wa Maji
5.Mamlaka ya Mapato(ukusanyaji wa kodi kuongezwa).
6.Tanesco (umeme wa uhakika ili kuimarisha uchumi na kukabiliana na wahujumu).
7. Kuondoa kero za Maliasili na Utalii.
8.Kufufua na kuanzisha viwanda vipya(walionunua bila kuviendeleza watanyang'anywa).
9.Kilimo, Ufugaji na Uvuvi(Tuna ng'ombe milioni 23 na kushika nafasi ya pili Afrika nyuma ya Ethiopia. Lakini tunaagiza bidhaa za ngozi nje ya nchi).
10.Afya; bajeti ya dawa itaongezwa, nidhamu ya watumishi, kila mkoa kuwa na Hospitali ya Rufaa. Hospitali kila wilaya. Zahanati kila kijiji na Kata.
11.Elimu bure kuanzia shule ya msingi hadi sekondari

12.Kupambana na Dawa za Kulevya.

13. Kuimarisha nidhamu ya utumishi wa Umma.
15.Baraza la Mawaziri kuwa dogo.
16.Kulinda Muungano.
17.Ujenzi wa Nyumba za Walimu.
18.Kukomesha Matumizi mabaya.
19. Kutatua kero, ujenzi wa nyumba za Askari na vitendea kazi jeshi la Polisi.
20. Kuondoa urasimu maeneo ya Mizani.
21.Kutengeneza ajira kwa 40%.
22.Viongozi walarushwa kutimuliwa na kushtakiwa.
23.Kupunguza safari za Nje.


 

 

THIS IS MAGUFUL TANZANIA PRESDENT


 Last weekend they were opening parliament and there was a state dinner planned for all guests that was going to cost about 300m. President Magulufi cut the budget to 25m and ordered that the rest be taken to buy hospital beds for Muhimbili they got 300 beds and mattresses and 600 bed sheets from that money. On 23rd Nov 2015 he announced that there will be no official ceremonies for Independence Day on 9th December, the money is to be used for more pressing issues and the day should instead be spent cleaning up our environment. On Saturday 21st nov 2015 a group of 50 people were about to set off for a tour of commonwealth countries (don’t know for what) but President Magulufi cut that list down to 4 people, saving government 600m in tickets, accommodation and per diems No more foreign travel, embassies will take care; if it’s necessary to go, special permission must be sought from him or Chief Secretary No more 1st class and business class travel for all officials except President, Vice, and Prime Minister. No more workshops and seminars in expensive hotels when their so many ministry board rooms available. President Magulufi asked how come engineers are given V8s when a pick-up is more suitable for their jobs. No more sitting allowances, how the hell are you paid allowance for a job which you have a monthly salary; that also applies to MP’s. President Magulufi has literally pressed the reset button; returning Tanzania to default factory settings, because that was the TZ Nyerere left us with. On the day after he was brought to power, in the morning as State House officials were showing him round he decided to take a walk to ministry of finance, told them to get their act together, asked why some employees weren’t in office (ever since then the traffic jam in mornings has become worse) and ordered TRA to scrap all tax exemptions, everyone must pay taxes especially the big guys President Magulufi went to Muhimbili Hospital unannounced and walked thru the worst parts that they keep hiding from important visitors he fired the director, fired the hospital board and ordered that all machines that weren’t working (so that people go to private hospitals owned by some doctors) to be repaired within 2 weeks otherwise he fires even the new director; the machines were repaired in 3 days Finally, last week when going to officially open parliament President Magulufi didn’t go by plane, drove the whole 600km from Dar to Dodoma. President Magulufi has reduced the size of the presidential convoy, even reduced the size of presidential delegation that travels with him President Magulufi chose a Prime Minister we haven’t heard of before, a guy with reputation for hard work and no corruption all the big guys we expected could be PM have been let wondering what hit them. His motto is: Hapa Kazi Tu After President Magulufi visited Ministry of finance and Muhimbii Hospital without announcing it is said the port (most corrupt, delaying, thieving officials) were all of a sudden the most efficient place. No loads are missing, things are done quickly and that habit of forcing for a bribe so that your container is released is no more. Oh, they say when he was confirmed as winner people started congratulating him and wanting to bring gifts to his place he turned them back, saying he will receive all congrats over the phone, nobody should visit him. All individuals/firms that bought state companies that were privatized but haven’t done anything (20yrs later) are to either revive the industries immediately or hand them back to the government

Sunday, November 29, 2015

ACHA DADA AOLEWE

Mawazo yake  dada ngu,anawaza kuolewa,
Ajikalie kwa chungu,moto wake kuchochewa,
Aoshe viombo  chungu,na sabuni atapewa,
Anawaza kuolewa,Anawaza dada yangu.
 
Atamania kuzaa,ajivunie  watoto,
Kamwe hawezi kata,autunze ujauzito,
Na dunia yashangaa,kulea kutunza wito,
Aolewe dada yangu,anawaza dada yangu.
 
Anatamani mapenzi,kitu hicho matatuzi,
Kinompa gugumizi,yu mpweke hana buzi,
Aibu kitu kishenzi,kiletacho uchokozi,
Chamnyima mume dada,anawaza dada yangu
 
Enyi vijana tulivu,namleta kwenu dada,
Wa mwenendo mkamavu,sanda kalawe kushinda,
Onesheni uangavu,kimpata tampenda
Ofa malumu naleta,anapenda kuolewa
 
Mwanaume na mwanamke,ndio nguzo ya umoja,
Wito mikono  tushike,tushikamane pamoja,
Ujasiri tujivike,familia kujengia,
Majukumu tujitwike,anapenda kuolewa
 
Ofa malumu naleta,wajunzi twanga pepeta,
Chelewaye sijejuta,sinambie sikupata,
Naogopa mi kusutwa,habari hiyo ni nyota,
Atakaye ameshinda,anawaza dada yangu.
 
Dada mwenyewe kigori,bikira ni mwanamwari,
Mrembo huyo mdori,mchapa kazi kijori,
Sura na rangi mzuri,msomi wa seKondari,
Elimu yake nasema,anawaza kuolewa.
 
Mwenyezi mungu kaumba,urembo nao kapamba,
Pendo jema si kasumba,namtangaza mchumba,
Tabia meitambua,mchapa kazi najua,
Sababu ni dada yangu,anawaza kuolewa.
 
Mfupi si mbilikimo,rangi yake kahawia,
Mashavuni na vishimo,nyuma tako katupia,
Hapaki tope domoni,nywereze ujisukia
Ni mrembo wa asilia,anapenda kuolewa
 
Hapatikani Asia,Hapatikani Ameika,
Zunguka zungu dunia,pande zote Afirika,
Watu wa kitanzania,binti huyo kaumbika,
kimpata taniambia,anapenda kuolewa
 
Hataki kuja chezewa,anataka kupepewa,
Ndoa ikishafungiwa,baraka mkigawiwa,
Muishi kivumiliwa,penye shida kutatuwa,
Mume na mke pamoja,mujeishi kwa umoja.
HICHO KIPAJI ULAJI
HICHO KIPAJI ULAJI,
MSHAIRI KAMA JAJI,
UKITUMIA UJUZI,...
FANYAYAKO MAPINDUZI.

YAPO MADARAJA CHINI,
YAKULA MOJA SAHANI,
WEWE KAMA MSHAIRI,
WATETEE KWA USHAURI,
YAPO MADARAJA JUU,
YANAYOPENDA MAKUU,
WENGINE NI VIONGOZI,
LAKINI NI MABAZAZI.
WEWE KAMA MJASIRI,
FICHUA ZA KWAOSIRI,
HICHO KIPAJI ULAJI,
MSHAIRI KAMA JAJI,
HICHO KIPAJIA UAJI,
TUMIA KWA MAUAJI,
UMASIKINI NA UJINGA,
MAGONJWA TAFUTA KINGA.
WATAZAME WAKULIMA,
TANGU ZAMA ZA UJIMAA,
WANALILIA MBOLEA,
YA SAMADI NA UREA.
MASOKO NAYO MAJEMBE,
ILI WALIME MAEMBE,
LAKINI KIPI WAMEEKOSEA,
FAIDA INAPOPOTEA.
MATAJIRI WENYE MALI,
WAPO WENGI SERIKALI,,
WANASURA ZA UKAFIL,
MAFISADI NA JEURI.
RUSHWA PAMOJA MAGENDO,
WAMEKOSEA UZALENDO,
FICHUA ZA KWAO SIRI,
NA KUWACHIMBIA KABURI.
HICHO KIPAJI ULAJI,
KIPAJI KANDAMIZAJI,
UKIFANYIE RISECHI,
KUMWOKOA MWANANCHI.
MYONGE NA MASIKINI,
WA MJINI NA KIJIJINI,
USISUBIRI NGOJA NGOJA,
JENGA ZAKO NGUVU HOJA.
VIONGOZI WAKIKUJA,
WATAULIZA MOJA MOJA,
KATOKAPI HUYO KIJAA,
MWENYE KIPAJI ULAJI.






PENZI BAHARI YA TOPE.
1.Penzi huvunja sharia, kwa mambo yalo magumu,
Zee la kuamkia, akupe umaamumu,
Tiba akikupatia, wapo wato kulaumu,...
Penzi bahari ya tope, haina mpiga mbizi.

2.Penzi huvunja sharia, zile za kimaumbile,
Kijura ukiyangia, tashika nyuma na mbele,
Zito takuinamia, hata upige kelele,
Maji yapande mlima, kwa mapenzi si neno.
3.Penzi hujenga ghorofa, pasina nguzo angani,
Mkwasi apose lofa, simba apende majani,
Maliki afe kifafa, kwa penzi la utumwani,
Nasema humpendaye, huhitaji kumsikia.
4.Penzi hupika chakula, bila moto tambueni,
Nahau Lila na Fila, ati havitengamani,
Fila kamuoa Lila, penzi lashindwa na nini?
Mja siseme hayawi, kwa penzi laweza kuwa.
5.Penzi huwa muujiza, bubu apate ongea,
Tena pia hushangaza, kiwete anatembea,
Kipofu anatangaza, mwezi amejionea,
Sishangae ndo mapenzi, bubu kuoa kipofu.
6.Penzi hutoka moyoni, si lile pande la nyama,
Penzi hisi za rohoni, ndo pumzi za mtima,
Penzi sione machoni, utakuja shika tama,
Nasema humpendaye, huhitaji kumuona.
7.Penzi si sauti nzuri, ya mahaba sikioni,
Moyo haufi kwa ghuri, zinazo kita ngomani,
Moyo ukiwa tayari, kiziwi atabaini,
Hata uwe na uziwi, sauti yake tasikia.
Dotto Chamchua Rangimoto.
Njano5.
255762845394whatpp
255784845394
 

MAPENZI TUYAPE PUMZI


MAPENZI TUYAPE PUMZI

Tuanze kama safari,twende mbali tukaone,

Mapenzi yetu hatari,nimeshazama nione,

Nitakupa hata gari mapenzi yetu yanone.

Mapenzi tuyape pumzi,yapumue kwa furaha.

 

Mapenzi tuyape pumzi yapumue kwa furaha,

tusije kuwa machizi,tukaishi kwa karaha,

tusifanye kama wezi,tupumue kwa furaha,

Mapenzi tuyape pumzi,yapumue kwa furaha.

 

Nakupenda si utani,usiniache jamani,

Penzi lako chini chini,nitulize kivulini,

Tusiyachome juani,tukajuta maishani,

Mapenzi  tuyape pumzi yapumue kwa furaha.

 

Usiwafate mabuzi,wakakuchuna na wewe,

Ukafanana na mbuzi,na sura mbaya ya mwewe,

Penzi letu ni mchuzi ,nimedata kwako wewe,

Mapenzi tuyape pumzi,yapumue kwa furaha.

 

Jamani kipenzi changu,ninakupenda moyoni,

Asali ya moyo wangu,sasa  shubiri ya nini?,                                  

Niponye nafasi yangu,nakupenda si utani,

Mapenzi tuyape pumzi,yapumue  kwa furaha.

 

Sina kinyongo moyoni,wala kiburi usoni,

Furahaa yangu machoni ,kicheko changu kinywani,

Papaso lako mwilini, lanipa joto jamani

Mapenzi tuyape pumzi yapumue kwa furaha.
.NIVUMILIE MPENZI.
Nivumilie mpenzi,katika shida na raha,
Mapenzi tuyape pumzi,yapumue kwa furaha,
Lidumu la kwetu penzi,liwe lenye nyingi siha
Nivumilie mpenzi,kwenye raha na karaha.
 
Penzi halina athari,subira likivutiwa,
Litakuwa machachari,mkazo likitiliwa,
Na mahaba ushamiri,bila ya kutarajiwa,
Nivumilie mpenzi,kwenye raha na karaha.
 
Penzi tuvumiliane,mahaba kuyafufua,
Suluhu ipatikane,kwa yanayo tusumbua,
Mengi tushirikiane,matatizo kutatua,
Nivumilie mpenzi,kwenye raha na karaha.
 
Nivumilie laazizi,mapenzi miangaiko,
Unipatie ujuzi,sielewi niendako,
Nina lingi jinamizi,jibu ushauri wako,
Nivumilie mpenzi,kwenye raha na karaha.
 
Penzi sio malumbano,penzi ni uvumilivu,
Wala sio mapigano,bali mwingi utulivu,
Penzi ni maridhiano,yenye kulitia nguvu,
Nivumilie mpenzi,kwenye shida na karaha.
 
Penzi si kwa masikini,wala halina chaguo,
haliitaji yakini,moyo ndio ufunguo,
likiingia moyoni,laweza kuvua nguo,
nivumilie mpenzi,kwenye raha na karaha.
 
Mapenzi uvumilivu,dawa ni uaminifu,
Dunia hii tulivu,kuna mengi mapungufu,
Penzi likikosa nguvu,hakuna uaminifu
Nivumilie mpenzi kwenye raha na karaha.
 

Saturday, November 28, 2015


SHOGA ACHA KUJIPWETEKA.

Shoga acha kujipweta, mume wangu sio wako,

Kutwa kucha kwa mwenzio, kwako wewe kunanini?,

Hujasikia kilio, wakuja kama utani,

Jioni na pulizio, tushakuchoka jamani,

Wewe si mke wa mtu?!,bado una wako ndani,

Shoga acha kujipweteka, mume wangu sio wako.

 

Shoga acha kujipweteka,mume wangu sio wako,

Vijana wanakujua, wamama pia wadada,

Jioni wawachukua, waenda kupaka poda,

Wasema umetulia, kijiko chako gireda,

Wewe si mke wa mtu?!, bado una wako ndani,

Shoga acha kujipweteka ,mume wangu sio wako,

 

Shoga acha kujipweteka,mume wangu sio wako,

Nadhani hujaelewa, Somo ninakupatia,

Usiku pombe kulewa, vijana wakupitia,

Nani asiyekujuwa, jilani na bi maria,

Wewe si mke wa mtu?!, bado una wako ndani,

Shoga acha kujipweteka, mume wangu sio wako.

 

Shoga acha kujipweteka, mume wangu sio wako,

Wataka mume wa mtu, magonjwa huya ogopi,

Wenzako vidudu mtu, wadanganywa nazo pipi,

Wewe si mke wa mtu, bado una wako ndani?!!,

Shoga acha kujipweteka, mume wangu sio wako.

 

Shoga acha kujipweteka, mume wangu  sio wako,

Vijana kuwachanganya, kesho huyu jana Yule,

Unakua kama panya, kulaga sana mchele,

Wazazi walikuonya, yataja  kukuta mbele,

Wewe si mke wa mtu, bado una wako ndani,

Shoga acha kujipeteka, mume wangu sio wako.

 

Shog acha kujipweteka, mume wangu sio wako,

Wenzako tuliwafunda, na sasa wametulia,

Majola na mama sonda, leo unawasikia,

Mume ni kama kidonda, siku utaja umia,

Wewe si mke wa mtu, bado una wako ndani,

Shoga acha kujipweteka, mume wangu sio wako.

 

Shoga acha kujipweteka,mume wangu siowako,

Ni kweli umetukela, waume kuwachukua,

Mimi na mama laila, wote twalalamikia,

Huu ni wako msala, lazima kuwachia,

Wewe si mke wa mtu, bado una wako ndani,

Shoga acha kujipweteka,mume wangu sio wako

 

 SHOGA ACHA UMBEA

Shoga acha ushangingi, shoga acha umbea,

Tadhani kunywa mitungi, na pia umeshalewa,

Au tafuna mirungi, domoni meelemewa,

Maneno yaso msingi, domoni umepaliwa,

Shoga acha ushangingi, shoga acha ushambenga,

Shoga acha umbea.

 

Shoga  acha umbea,shoga acha ushangingi,

Kutwa kucha watembea, machoni mepaka rangi,

Kuchonga na kuchongea, hata visivyo msingi,

Domo lako melegea, guu limeota gigi,

Shoga acha ushangingi, shoga acha ushambenga,

Shoga acha umbea.

 

Kwani watulisha sie, au  watuvisha shoga,

Tuache tujikaangie, miogo hata maboga,

Mavazi tujivalie, tupendeze kwa kukoga,

Ewe mbea ulie, tafurahi kijinyonga,

Shoga acha ushangingi, shoga acha ushambenga,

Shoga acha umbea.

 

Kutwa kucha kuchunguza, kutwa kucha kupeleleza,

Vijana wabembeleza, wataka kuwapoteza,

Jahanamu kwenye kiza, nenda mwenyewe kuoza,

Shoga acha ushangingi,shoga acha ushambenga,

Shoga acha umbea.

 

Bwana asie wa kwako, wamtakia kinini?,

Walegeza jicho lako, wamvalia kimini,

Watingisha lako tako, lainika kiunoni,

Na vingi vingi vituko, umtupe kitanzini,

Shoga acha ushangingi, shoga acha ushambenga,

Shoga acha umbea.

 

Tuliza wako mtima, katulie sebuleni,

Uache kutuchochoma, kama nyama ya jikoni,

Kwani unavyo loloma, faidaze huzioni,

Jitafutie heshima, utapendwa abadani,

Shoga acha ushangingi, shoga acha ushambenga,

Shoga acha umbea.

 

Nenda shamba ukalime, matunda utayapata,

Wanini hao waume?, ambao unawafata,

-hghWengine mapaka shume, utapigwa utajuta,

Mara ukishikwa shime, ngumi zitakukumbata,

Shoga acha ushangingi, shoga acha ushambenga,
Shoga acha umbea.