Monday, March 24, 2014


       SEHEMU YA PILI

Siku iliyofuata  boga akamwambia dady anaenda kwenye mashindano talent show,dady hakua na kinyongo akamkubalia mwanawe na pia alipomwona pamera alifurahi sana kwani pamera alikua ni binti mchangamfu na Mwenye furaha na pia alikosa aibu kabisa,pamera na boga wakaenda mwenge pamera akiwa amemshika boga mkono  wakayacheki majina yao kwenye notice board kwa bahati nzuri wote wawili walibahatika kuingia kwenye yale mashindano,walichaguliwa vijana therathini.

Vijana wote wakatambulishwa kwa hadhira iliyokuwepo pale kwenye hall,msemaji mkuu au msema chochote wa siku hiyo alikua ni Mc maharufu kwa vitimbwi vichekesho pamoja na vituko vya hapa na pale  MASANJA MKANDAMIZAJI  Pamoja na mchezesha music almaharufu kwa jina la DJ CHOKA .Lakini pia ukumbi ulipambwa na vifaa vya kimuzic kama vile magitaa,matarumbeta,vinanda,violin,ngoma za asili na vifaa vingine vingine vingi bila kusahau microphone pamoja na speeker kwa ajili ya kutole  na kuingizia sauti.

Yalizaliwa makundi sita kila kundi liliwabeba vijana watano watano kundi la kwanza liliitwa HARDER TO TOUCH, kundi ili liliwabebavijana wa kiume watatu  na wa kike wawili majina yao waliitwa MIZANI,KINOMANOMA,GODZILLA,MAMAJUSI,na RWANDAI. Kundi la pili liliitwa  WAKARI CLASSICS kundi ili liliwabeba vijana kama vile BENITOTO,ALL DAYZ CONFIDENCE,NAIROBI,YOUNG MBARA, na ELIA ABELIA. Kundi lao liliwabebe vijana wote wa kiume.Kundi la tatu lililoitwa  LAZIMA TUSHINDE liliwakusanya vijana kama vile MALIPO MARIBORO,LERATO,PANDA HILL,MAMA SILVANO, na ANDUNJE,

 Kundi la SISI NI BALAA liliwazoa  wasanii wake majina yao ni JOHSON JOHN,SISTER ABELLA,ADAMSON ,NEEMA MWAKYUSA na DIANA NYOKS, achilia mbali majina ya kundi hili kundi la tano lililoitwa SIMBA DUMEZ NA SIMBA JIKEZ liliwakusanya wajanja wake kama vile IRENE POO,GOD LISTEN PETER JOSEPH,SABA SABA,NDANDA NGABI na SHAA DIANA ROZE, kikundi cha mwisho wao walijipa jina la  HAMTUWEZI  hawa walijipanga vizuri  kwa majina yao kama vile PAMERA,BOGA TALENTER,POMONI DIA,COMMOROW na LOSHORO 


Mc masanja mkandamizaji akawaambia kuwa wote pale hawapo kuuza sura zao(kujionesha tu) ila wapo palekuonesha vipaji vyao vya hali ya juu,uwezo ubunifu juhudi pamoja na kujituma kwao ili waweze kushinda mamilioni ya shilingi  na kuitangaza vizuri ramani ya nchi yetu kimataifa.Wote walitakiwa kushiriki au kushirikiana katika categorization mbali mbali zikiwemo

                               1.MAPISHI YA VYAKULA VYA AINA MBALIMBALI

                                2.UFUNDI WA KUBUNI MAVAZI YA AINA MBALI MBALI(fashion show moder)

                                3.MAIGIZO

                                4.KURUKA KAMBA

                                 5.KUOGELEA

                                 6.MUZIC(kuimba,kucheza,kutunga na kushirikiana katika performance)

                                 7.UBUNIFU KATIKA UCHORAJI

                                 8.UREMBO NA UTANASHATI

                                 9.USAFI KWA UJUMLA

                                 10.KUKIMBIZA BAISKERI KWA MIGUU

                                 11.KUVUTA KAMBA

                                 12.MPIRA

                                 13 KUKIMBIA,.KUKIMBIZA KUKU, KULA NA KUNYWA

                               14.UBUNIFU WA KUJIBU MASWALI KWA LUGHA YA KIINGEREZA

                                 15. MAZOEZI YA VIUNGO NA MAPAMBANO


                                         MAPISHI

Siku ile vijana walipewa kazi moja tu ya kuandaa mapishi  ya aina mbalimbali kila aina ya vyakula ililetwa hapakukosekana aina yoyote ya chakula kwani hata wasivyovijua vililetwa mbele yao vikiambatana na viungo mbalimbali vya hayo mapishi bila kusahau mafuta chumvi,au sukari ili kufanya vyakula viwe vitamu.Zikaletwa mbele yao

cabbage,Chinese,spinach,carrot,matango,spagget,unga wa kupikia vyakula vya aina mbali mbali ikiwemo ugali na mikate ya ngano,samaki.mchele, nyama ya kuku ya nguruwe ya mbuzi ya bata, dagaa,sukuma wiki, mnafu,ngogwe,njegere,kunde bamia,na vinginevyo vingi pasipo kusahau matunda. Sasa kazi ikaanza kila mtu aliitaji kushiriki vizuri ili kuleta mvuto wa kazi ile.Wakapewa mavazi maharumu kama yale ya wapishi wa mahoteini nao wakajivika vema wakaonekana  kama wapishi haswa.

Sheria iliyowekwa ilikua ni kwamba iwapo kundi moja limeshindwa kufanya vizuri au makundi yote yameshindwa kufanya vema kwenye yale mashindano basi watu wote wakundi au makundi husika walitakiwa kufungasha virago na kutokomea kurundi Nyumbani kwao.

Kundi la Harder to touch kama walivyopenda kujikita wenyewe  YOU NEVER TOUCH US,lilikua ni kundi la vijana wachangamfu,wacheshi,wapole na pia vijana wenye matumaini sana ya kushinda kwa swagga zao hata siku ya kwanza kupanda jukwani hadhira iliwshangilia mno wakijipa matumaini ya ya kwamba ushindi ni wao hakuna wa kuwazidi na watashinda kwa kishindo kikuu cha kushitukiza.

Haraka haraka wakapata wazo kuwa waandae mlo unaoitwa LOSHORO,pishi la kabilala watu wa kaskazini mwa Tanzania maharufu kama wameru wa Arusha. Wao walichofanya walichukua ndizi ambazo hazijaiva yaani matokii,wakaumenya mkungu mzima wa zile ndizi za matokii kisha wakazikata kazikata vipande vipande baada ya kuzichemsha ndizi zile wakakata nyama vipande vipande nazo wakazichemsha,wakachukua mahindi ya kukobolewa nayo wakayachemsha vizuri vyote vikawa  vinatokota tokota na kutoa harufu nzuri ya utamu na unono na baada ya kuona kuwa pishi limeivaa

 wakachanganya na maziwa mgando,ila walipenda sana kutia maziwa fresh lakini ilikua nichaguo  lao wenyewe……….kwanza kabisa waliziponda ponda zile ndizi zikawa uji uji na kisha `wakachanganya na nyama bila kusahau yale maziwa pamoja na makande pishi likaendelea kutoa unono.Hakika lile pishi lilikua ni pishi bomba kisawa sawa ingawaje walisahau kutia chumvi ilo nalo likawa kosa lao kubwa sana.

Pishi la pili walilolizimia kulipika lilikua ni pishi la chapatti maharagwe,chai nzuri ya maziwa freshi ikatengenezwa maziwa mazito ya moto moto yakachemshwa chapatti tamu aina ya chapatti kavu zikapikwa pamoja na maharagwe yalikaangwa vizuri.Upungufu wao ni kwamba walisahau kutia kiungo mahalumu kiitwacho nyanya ingawaje mafuta  ya kula,pilipili hoho,caroot pamoja na vitunguu viliwekwa vizuri.mbali na ilo pishi  pia chai yao ilikosa sukari jambo ambalo wao wenyewe kama kundi walisahau kutia sukari.

Pishi la mwisho walilolipika lilikua ni pishi  la ndizi za kukangaa zilizotiwa asali,chips mayai,viazi mbatata vya kukaangwavilivyotiwa pilipili,baada ya kumalizia mapishi yao wakayaifadhi mahari pazuri kisha wakapewa ruhusa ya kuondoka ili kupisha kundi la pili nalo lioneshe mahanjumati yake,kwani hadhira ilivutiwa sana na juhudi pamoja na ujuzi ambao kundi la  HARDER TO TOUCH  liliuonesha.

Likapewa nafasi kundi matata na kundi machachari la la WAKARI CLASSICSS ingawaje ndani ya kikundi hiki walikuwemo baadhi ya vijana wenye tabia chafu kama vile unywaji pombe kupita kiasi,uzinifu ,kutukanana matusi ya nguoni,kupigana na pia kuibiana vitu,lakini vijana walikua wapo super wapo juu katika kujituma na pia kufanya maujanja ya hapa na pale.Walijinadi kua wao ni wakari na hakuna mtu wa kuwazingua,kwani wanaweza kuliambia jua simama nalo likasimama,wanaweza kuliambia jiwe badirika uwe mkate nalo jiwe likabadirika,bahari iwe chumvi nayo inakua chumvi,nyoka awe samaki naye akawa samaki.Walijigamba na kujinadi sana hadi hadhira ilipasuka mbavu kwa vicheko mfululizo.


Wao walikubaliana kuandaa UGALI WA MAZIWA FRESH YA MOTO,ugali ukapikwa kwa kutumia unga wa dona na maziwa fresh yakachemshwa.pishi la pili  lilikua ni mboga mboga wao walichofanya ni kutengeneza cabbage ya kuchemsha na kutia aina zote za viungo, mchuzi wake wakauweka pembeni na walipoulizwa mchuzi wa cabbage una saidia nini mwilini jibu walilo litoa ni kuwa mchuzi ule ni mzuri sana kwa  kupunguza mafuta na unene mwilini.


Walipomaliza hiyo shughuri pevu pishi lililofuata  lilikua ni mayai , mayai haya waliyagawa katika makundi matatu kundi la kwanza lilikua ni mayai ya kuchemsha  wakatengeneza na chai ya maziwa wao walisema kuwa mayai ya kuchemsha pamoja na maziwa usaidia kupunguza unene mwilini.


Lakini walipopika mayai yaliyochanganywa na vitunguu,carrot, pamoja na vipande vya hoho walidai kuwa haya ni mazuri kwa ajiri ya kunenepesha mwili na kuupa mwili nguvu pamoja na akili. Wakamalizia kwa kupika mayai yaliyo changanywa na carrot nyanya na hoho ,vitunguu  pamoja na samaki watatu waliokaangwa kisha mapishi ya kuchanganya changanya vile vitamu tamu yakaanza.shughuri ile pevu ilipoisha walivitandaza vyakula vyao vitamu mezani ili hadhira ipate kuonja kunusa nusa ,kububuna,kukodorea macho, kuvitamani na kujifunza zaidi kutoka kwao kwa kutumia maswali na majibu juu ya utundu na utaalamu wao katika mapishi.


Kundi la tatu la LAZIMA TUSHINDE na KUNDI LA SISI NI BALAA  ambalo ni kundi la nne wakaitwa wote kwa pamoja ili kuonesha hadhira manjonjonjo na mautundu ambayo mwenyezi Mungu amewajalia hawakua na makuu sana  upole busara wema na kujituma ndiyo ilikua sifa yao njema.Walianza na uhandaaji wa juisi ya matunda,hatua ya kwanza waliyoichukua ilikua ni kutafuta maembe,maparachichi,machungwa,maboora


mapapai,mananasi,na matunda mengineyo mengi ya shambani kisha wote kwa pamoja wakayamenya vizuri tena kwa wingi utadhania mchango wa baharini na hatua ya tatu ilikua ni kuyasaga kwa kutumia mashine maharumu ya kusagia matunda kwenye jagi, na hatua ya mwisho ilikua ni kuyaifadhi yale matunda kwenye chombo maalumu kila spice ya matunda kwenye chombo chake na mahari pake.


Pishi la pili lilikua ni pishi la uji(stiff polidige)uji mzito ulitengenezwa,uji uliochanganywa na maziwa freshi mazito ya ngombe ,ukitegemea walitumia utundu na ufundi wao kwa kuchanganya blue band,karanga, mahindi,njegere choroko mtama ulezi,maharagwe ya soya, mchere na ngano.kwa pamoja vilisagwa vizuri vikachanganywa changanywa uji mzito uliotiwa sukari ya kutosha uliwekwa tayari kwa ajiri ya mywaji.


 Wakamalizia kwa kupika pishi bomba haswa wala sio lingine bali ni pishi la  la supu ya  mafuta mafuta ya ngombe yalochanganywa na nyama kadha za mbuzi, wakapaliliza na nyama ya kondoo si mchezo kwani hawakusahau nyama ya kikanda cha nguruwe,kweli mtu ni afya na ni lazima ale vyakula bora.


Likaitwa kundi la tano  kundi la SIMBA DUMEZI NA SIMBA JIKEZI ,vijana hawa hata ukiwaangalia hakika usingesita kujisemea hawana mpizani,vijana walijariwa urembo na utanashati na pia nguvu zao za kuchapa kazi zilikua hazihesabiki ,ndio  maana wakajiita simba dumezi na simba jikezi, maringo ndio ilikua sifa mahususi ya kundi hili, waka         yavunja moyo makundi mengine lakini ukweli ni kwamba asokubali kushindwa si mshindani.


Nyama ya kuku ikaandaliwa,wakai rostisha ile nyama.Nyama ya ngombe ikaandaliwa mchemsho safi sana,nyama ya mbuzi ikaandaliwa mishikaki bomba haswa na pia nyama ya kondoo ikapikwa vizuri vizuri kwa kutumia viungo vitamu vitamu bila kusahau pishi bomba la dagaa wa ziwa Victoria dagaa wanene na tena wenye afya kama mlima Kilimanjaro.


Pishi la pili lilikua ni pishi la  mboga za majani wakajiandalia Chinese safi ya kukaanga kwa mafuta tu,wakakata kata mnafu na kuchanganya pamoja na ngogwe,ingawaje vyakula hivi ni vikari lakini walitumia utaalamua wa hali ya juu kuviandaa ili kuhakikisha ya kwamba pishi lao halina dosari yoyote ya ukari,achilia mbali  pishi lao la mboga mboga kama vile mchicha, mrenda waliotia bamia magadi maharagwe pamoja na mboga mboga za majani,pamoja na hayo yote walipika njegere kavu choroko kavu na kunde kavu……..ama kweli vyakula bora ni dawa kwani ushindani ulikua ni mkari.


Na pishi walilolimalizia lilikua ni utengenezaji wa matunda. Matunda yao yalikua ni mchanganyiko wa vipande vipande vya carrot,maembe,hoho,nyanya,vitunguu,ndizi za kuiva,matikiti maji,rimon,matango,maparachichi,matunda damu, na maembe baadhi ya matunda waliyachanganya changanya na na mengine waliyakata kata hivyo hivyo tu na kuyaifadhi kwenye vyombo maalumu safi.


Hakika hadhira ilifurahishwa sana na juhudi nguvu na uwezo wa kubuni mambo mazuri ya jikoni yaliyofanywa na kundi hili watu wengi sana waliwapigia makofi na kuwapatia kura nyingi sana kundi la SIMBA JIKEZI NA SIMBA DUMEZ,wali wapooza kwa kuwaambia maneno mataamu ya kuwatoa nyoka mapangoni kwamba ushindi ni wao bahati yao imegonga mlangoni wala wasiiache ikapita na kwenda zake.


Kundi la mwisho ambalo ndilo alilokuwepo boga talenter pamoja na pamera,lililojurikana kwa jina la HAMTUWEZI wakapita ukumbini kama vile rocket iendayo kwa kasi ya mkorea,hawakua na haja ya kupita kama vile vinyonga wenye njaa,ingawaje hawakuleta mvuto kwa hadhira ile kundi ili lilijaa vijana wenye aibu na soni ila tu baadhi yao walikua super  wana nyota za mvuto.


Walichofanya wao  kama kundi walikubaliana kuandaa chakula cha jioni kwanza. Pilau iliyo sheheheni  viazi mviringo pamoja na nyama nzito ya bata mzinga pamoja na kuku aina ya kanga  zilipikwa vikanukia sana hadi hadhira ikaanza kumezea mate harufu tu ilitosha kushibisha ile hadhira. Walipomaliza shughuri ile wakaunganisha na wali mweupe uliotiwa nazi,carrot,maharagwe na pia wakakoleza kwa kutia asali iliyoogeza utamu hadi kwenye visogo vya hadhira.


Pishi la pili lilikua ni pishi la spagget  au kwa jina lingine tambi hapa napo waliwashangaza watu kwa maajabu yao makuu waliyo ya fanya kwani watu wengi sana hawakujua jinsi ya kupika spagett sasa siku ile waliamini kuwa duniani kuna  watu wataalamu na wajuzi wa mapishi.Kwanza  spagget au tambi zikakatwa katwa vipande kisha zikatiwa kwenye maziwa yaliyokua yanachemka baada ya kuiva zikakaangwa kwenye mafuta na baada ya shughuri ile pevu spagget zikawekwa karrot zilizo sagwa vizuri pamoja na vitunguu na baada ya pishi ilo tamu likapalilizwa kwa mboga mboga za majani juu yake wakaweka maua yalonukia na kuvutia.


Walipolimaliza ilo pishi safari hii wakaunganisha na pishi la vitafunwa vya staftahi hapa washiriki wakalipa jina ili pishi siku njema ionekayo asubuhi,wakachanganya unga wa bakery kidogo wakatia na unga wa ngano,keki ilotiwa chocollate ikaandaliwa,mkate mtamu wa ngano sijui wanaita BUMUNDA likapikwa, maandazi aina ya donate yakawekwa pale mezani,vipande vya bisscut na karanga za kukaangwa  zikawekwa kwenye sahani ndogo ndogo ziitwazo visosa.Hawakusahau kutengeneza chai ya maziwa,ya rangi, ya kahawa naya cocoa.


Wakapewa tena nafasi ya kuandaa  pishi la mwisho hawakua nyuma katika kuandaa pilipili ya kiutamaduni wao waliipachika jina la  traditionar peeper hii ndio pilipili inayotengenezwa kwa kusaga nyanya  kwa kutumia mashine maharumu ya kusagia,mpaka nyanya zinakua kama maji maji,wakachanganya pilipili iliyoitwa pilipili mbuzi kisha wakachanganya na pilipili moja kari kwa jina la pili pili  kichaa.


Amakweli kazi ya mapishi ni kazi ngumu sana zio kazi ya kuwaachia wanawake tu waishughurikie wakiwa Nyumbani bali ni kazi inayoitaji ushirikiano kati ya mwanaume na mwanamke,kwani umoja ni nguvu utengano ni udhaifu,zoezi ili gumu utadhania watu wana ng’oa mlima Kilimanjaro kwa mikono yao likaisha vizuri sana.


Msemachocote(Mc)wa siku ile ndugu Masanja Mkandamizaji aliwapongeza sana washiriki wote kwa jinsi walivyoonesha


juhudi zao,nguvu ushirikiano pamoja na uwezo wa kiubunifu kwani utaalamu walo uonesha ulitosha kudhihirisha kuwa  wapo juu kinoma.pia aliwapa pole kwa kazi nzito kama ile akawatia mioyo kuwa wavumilivu kwani ni hadhira pamoja ma majaji ndio walikua na haki ya kusema neno la mwisho

“ wewe bakia au wewe ondoka”

ni aina gani ya mapishi ina changamoto,udhaifu,au mapungufu, ni aina gani ya chakula kina radha,tija,harufu,afya,unono utaamu na pia je kinapendeza kuliwa au la hasha.


Hadhira(watazamaji au wasikilizaji au mashabiki)ikaitwa mbele ili kuanza kufanya utafiti wao kwa kila chakula, makundi yote yakawekwa pembeni ili kupisha hadhira kujipakulia kujichotea kujimiminia na kujichana kwa kujilia mautamu yale yalo andaliwa pia kuchangia mawazo kwa kutoa changamoto mapungufu na madhaifu ya kundi husika.Kundi la Harder to touch likapewa nafasi ya kuonesha utamu wa manjonjonjo yao hadhira iliyokuwepo pale haikusita kusema kuwa  chumvi haikutiwa kwenye chakula aina ya loshoro na pia nyanya


hazikuwekwa kwenye  kwenye maharagwe,ingawaje walijitetea kwa kusema kwamba maharagwe yakitiwa nyanya yanaweza kuchacha ilo nalo likaibua maswali mbele ya hadira wapo waliokubali na wapo waliopinga vikari.


Kundila pili nalo likafanyiwa assessment kundi ili lilibahatika kupita paso udhaifu wowote la tatu na la nne nalo  yakafanyiwa research yote yaliibuka paso matatizo kundi la tano pia halikua na any problem lakini watu walilitilia mashaka kundi la sita ingawaje halikua na kasoro nyingi sana  ila tu hadhira haikuona kama kundi ili lina mchango mkubwa kwenye mapishi yake.


Msema chochote akaishukuru sana hadira kwa ushirikiano waliouonesha katika kufaidi na kutoa mawazo yao kulingana na changamoto au pongezi la pishi la kundi husika,kundi la pili na la tatu,la nne na la tano yakapongezwa zaidi ila kundi la  la kwanza na la sita yakawekwa kikaangoni sasa ikawa ni zamu ya hadhira, kupiga kura ili kuangalia kati ya makundi hayo mawili kundi la Harder to touch na kundi la Hamtuwezi ni lipi lifungashe virago ili liyaage mashindano yale hadimu.


Mamia ya watazamaji wakapewa nafsi ya kupiga kura vipande vidogo vidogo vya karatasi vikaretwa na kila mtu pasipo ubaguzi wowote alipewa nafasi ya kuandika ni kundi gani kati ya harder to touch na la hamtuwezi yalifaa kufungasha virago vyake na kuondoka.hadhira wakapiga kura zile kimya kimya na baaada ya kumalizia  upigaji wa kura zile zikapelekwa kwenye panel ya majaji sita wa hayo mashindano,panel ikakaa kuhesabu kura  mbele ya wahusika wote na watazamaji wote.


Kwenye meza ile ya panel ya majajaji  walikaa watu maharufu Tanzania bara na visiwani  Zanzibar achilia mbali umashuhuri wao ulivuka mipaka mpaka nchi mbali mbali za Africa mashariki na Africa ya kati ,Kenya Uganda Rwanda Burundi Zaire Malawi na Zambia.Pannel ile wali upande wa kuria  kiti cha kwanza alikaa mtangazaji maharufu kwenye kipindi chake kinachoenda kwa jina la MKASI na kinachorushwa na televisheni kubwa Africa mashariki


SALAMA JABIRI diva anaye wahoji na kuwatwanga maswali mawili matatu wasanii na watu maharufu Tanzania na Africa mashariki kama vile wakina Ambwene yesaya(AY) REHEMA CHARAMILA (RAY C) Mrembo wa Africa NANCY SUMARY na dadaye mwanamuzikia NAKAAYA SUMARY na wengineo wengi tu kwani hawa ni baadhi yao.


Mtu wa pili upande ule ule wa kuria alikaa MAADAM RITTA PAULSEN huyu naye alikua mahuhuri kwa kuwato wasanii mbali mbali ndani na nje ya Africa mashariki wabunifu na watu wenye vipawa pamoja na vipaji vyao  kwa kutumia kampuni yake ya BENCH MARK PRODUCTION. Bila kumsahau mwana dada wa kipindi cha  WANAWAKE LIVE kipindi kinacho onesha mabo mbalimbali ya wanawake wanavyojituma katika shughuri za kimaendereo


kiujasiliamali, mwanadada huyu mtetezi wa wanawake na watoto  alisifika sana katika kuangalia changamoto wazipatazo wana wake,migogoro inayo wakumba wana wake katika kulisukuma gurudumu la maendereo, uhusianao bora kati ya wana wake na wanaume katika ujenzi wa familia bora zaidi duniani,malezi mema kati ya mama na  mtoto na mambo mengine kem kem.si mwingine bali ni mrembo wa Africa mashariki na duniani kwote JOYCE KIRIA.


Upande wa kushoto waliketi wana ume watatu kwanza alikuwepo MASTER JAY mwanaume huyu Mwenye sura ya upole hekima aibu na wema ulo mtawala.huyu ni producer maharufu BONGO kwa kumiliki studio yake inayo kwenda kwa jina la MJ RECORDZ,achilia mbali uwepo wa master jay pia alikuwepo msomi aliye bobea katika  masuala ya michezo,elimu sanaa na utamaduni ubunifu na vipaji hakua mwingine bali ni muheshimiwa ndugu WAZIRI WA ELIMU MICHEZO NA UTAMADUNI si mwigine bali ni  PROFFESOR PATRIC MULLUNGU. Mtu almaharufu Tanzania bara na visiwani kwa hoja zake ziloshiba awapo bungeni akiitetea elimu kuwa ndio ufunguo wa maisha,ndio bahari ya mafanikio,ndio kitu kisicho na mwisho,ingawaje mwanadamu ana mwanzo na mwisho wake lakini elimu imekosa mwanzo na mwisho wake.


Na judge wa mwisho kabisa aliye keti katikati hakuwa mwingine bali ni mtu mdogo kiumbo ila ana mambo makubwa katika fani na tasnia nyinginezo za sanaa kama vile tamthiriya,filamu,maigizo, na vichekesho aina ya commedy Tanzania bara na visiwani Zanzibar .huyu ni mtu maharufu ambaye sanaa yake ipo kwenye kila kipande cha nyama zake ndani ya damu na ndani ya mishipa yake ya fahamu si mwingine bali ni msanii anaye kwnda kwa jina la KIKONGWE  JOTI ,au kama wamwitavyo watazamaji wa television ya  TBC, ASHA NGEDERE kila jicho la mwafrica umtazama asha ngedere siku ya jumataano na juma pili.


Hao ndio panel ya majaji walokaa chini na kuanza kuzi calculate zile kura  kwa uhaminifu mkubwa kwani wote walikula kiapo cha kutodanganya neno lolote wakiamini kuwa msema kweli ndie mpenzi wa Mungu kura zile zikahesabiwa alfa na omega baada ya mchakato mrefu kama vile kamba iendayo angani kuuvuta mwezi pasipo mafanikio hatimaye haki ikatangazwa.katika mchakato wa kuwapata washindi wa mashindano haya kundi la wakari classics wakapewa nafasi ya  kwanza kuwa ndio kundi bingwa kwa kuyashinda makundi yalofuati.


Kundi la samba dumezi na samba jikezi likapewa  nafsi ya pili ya ushindi kwani lilionekana limefanya poa sana mbali na hapo kundi la tatu na la nne ambapo kundi la tatu lilitwa lazima tushinde na kundi la nne lilitwa sisi ni balaa yote kwa pamoja yakapata nafsi ta tatu kwani yaliungana na kufanya kitu kimoja.pishi zao zilitia fora sana kwa mahanjumati yalotokota yalonukia yalo kua manono matamuuu yaani very delicious.


Kundi la tano la hamtuwezi liliopewa nafsi ya nne ya ushindi ingawaje kundi lile la kwanza la harder to touch lilivurunda na kupewa asilimia chache hatimaye haki ikatangazwa  kuwa kundi la harder to touch  lifungashe virago lishike njia kwa kutumia miguu yake.hatimaye kundi la harder to touch likafungasha virago kwa huzuni utadhani kinda aliye tekelezwa na mamaye kwani walimwaga kilio na kusaga meno utafikiria nafaka zinavyosagwa kwenye mashine.


Makundi yalosalia yakapongezwa sana na kupewa nafsi ya kujisukuma zaidi kwani daima mbele nyuma mwiko hiyo ndio ilokua point ya msingi......
itaenderea sehemu ya tatu
usikose......


                                         

No comments:

Post a Comment