Monday, March 24, 2014



 STORY       MASHINDANO TALENT SHOW


 WRITTEN BY   ELIA ABEL MWALUKALI             


WRITTEN IN   ARUSHA (USA RIVER)


STORY WRITTEN ON    MARCH 2014


               Story ya kwanza


 


         MASHINDANO TALENT SHOW


SEHEMU YA KWANZA



DAR ES SALAAM TANZANIA  



Ilikua ni  hasubuhi  ya saa tano na nusu  nyimbo za music wa kitanzania  zinazopendwa sana  na vijana wa kizazi kipya almaharufu kama bongo fleva zilikua zina sikika kwenye televisheni kubwa yenye screen ya rangi nyeusi ikiambatana na midundo mikali hasa ya huo muziki, midundo inayoweza kumto a nyoka pangoni ihari nyoka hataki kutoka.kijana mdogo Mwenye umri wa miaka ishirini alikua amelala usingizi wa fofofo,pembeni ya kitanda kile alilala mbwa mdogo mmoja mweusi  na huyu kijana alijulikana kwa jina la BOGA TALENTER.


Akaja babaye  akamwita kwa sauti kubwa sana utadhania kipaza sauti ;


“boga…….boga…..boga…….. “


lakini boga alienderea kulala akinguruma kama vile  simba mwenye hasira.babaye Mwenye umri wa miaka 45 mrefu mnene,bado alionekana kuwa kijana  smart Mwenye mvuto wa kipekee ukitegemea msomi yule alifahamu umuhimu wa kula vyakula bora vinavyotia nguvu mwili pamoja na akili.


Babaye boga akaenda kwenye jokofu akachukua maji ya baridi sana  taratibu akarejea kwenye chumba cha  cha mwanae boga talenter  akafanya uhamuzi wa kumwagia maji  ya baridi  palepale kitandani,yallab mola maji yalikua ya baridi haswa utazania barafu  za milima ya ulaya,boga akashituka mshituko mkuu ulioambatana  na kukurupuka pale kitandani akiwa anatetemeka pamoja na kukamua nguo yake iliyolowa kwa maji yale ya barafu.


Babaye boga akamwambia kwa ukari


Boga kwanini unalala mpaka  saa hizi badala ya kuamka ili ufanyie makazi yote usafi.vyoo vilinuka,nyumba ilichafuka,viwaja vilioza,maua yalinyauka lakini boga hakupenda kila siku kujishughurisha na shughuri za usafi wa nyumba.Siku ya jana boga talenter alijisaidia chooni,lakini kwa bahati mbaya alijisaidia pembeni na pia hakumwagia maji choo ukitegemea choo kilikuwepo ndani,harufu kali ilijipenyeneza sebuleni kwao na kuwa kero kubwa sana kwa babaye mzee talenter liyekua anafanya kazi kwenye kiwanda cha kutengenezea nguo cha URAFIKI DAR ES SALAAM.


Babaye akiwa amefuraa kwa hasira akamuuliza boga kwa nini tabia yake ni mbaya namna ile,kwanza amejisaidia pembeni ya choo na kwa makusudi  akiwa anaelewa kuwa maji yapo ndani ya choo na pia toillent paper zilikua nyingi tena za kumwaga .Boga alishindwa kulijibu lile swali hapo ndipo hasira za babaye zilianza kuwaka kama cheche  za moto wa tanuru.Babaye akamchukua boga na kumweka kwenye kiti kirefu,viti vile vitumikavyo kukalia mezani muda wa kula chakula cha kifamilia akamwingiza ndani ya kile kiti na kumgeuzia kwenye televisheni screen, huyo akaerekea nje akiwa anaongea pekee yake “naenda kuchukua fimbo mjinga mkubwa we”.


Kichwa cha boga talenter kiliangaliana na televisheni screen,ghafla televisheni ile ikaacha ku play muzic yakafuatia matangazo likaonekana tangazo mtangazaji akitangaza kwa mbwembwembwe kubwa.


         “ mashindano talent show,kama wewe ni kijana mtu mzima au mzee Mwenye kipaji au ubunifu             wowote ule wa kuionesha jamii nini mwenyezi Mungu amekujaria njoo uioneshe jamii na mwisho wa mashindano talent show mshindi au washindi atajinyakulia au watajinyakulia  pesa tasilimu milioni mia nane…..waoooooo………”.


mtangazaji akaenderea;


“ fomu zinapatikana barabara ya mwenge eneo la bamanga karibu karibu na ofisi za kampuni ya habari na mawasiliano ya GLOBAL PUBLISHERS mamilion ya pesa yatashindaniwa,wahi sasa nafsi ni chache”.




Baada ya kumalizia lile tangazo yakarushwa mamiliion ya  pesa kwenye kioo cha televisheni.


Ghafra boga akahisi kama kuna kitu kimempasukia  nyuma kwenye makario yake maumivu makari  aliyasikia yaliyoambatana na uchungu  aliousikia kumbe babaye alianza kumcharaza viboko vya nguvu pamoja na kulalamika kuwa siku hizi boga amekua na tabia mbaya tena isiyofaa kuigwa kwani kuoga mwilini haogi,kufuta deki chumba chake hafuti hata akiambiwa hawezi kuitii au kuisikiliza sauti ya babaye, mtoto anawaza kula na kulala,sasa amejisaidia chooni je ni nani atakaye hangaika kwenda kusafisha kile choo zaidi ya mshenzi mwanaharamu yule boga talenter.Babaye akamtandika viboko kumi na viwili,boga alilia sana,baba nisamehe sitaweza kurudia tena,nimekosa najuta nimekosa sitorudia tena.


Hasira zilizidi kumuwaka babaye boga talenter safari hii akautwaa mkono wake na  kuupachika kwenye sikio la boga talenter maumivu makari yaliyoambatana na churuziko la damu kwenye sikio ndiyo aliyo yasikia bogatalenter,babaye akamvuta boga talenter mpaka nje ya lango la getini kisha akamsukumia nje boga, boga akaanguka na kuhumia vibaya sana kwenye got lake la kulia churuziko la damu nalo likafuatia, babaye Mwenye hasira za mkizi akamwambia boga;


“kuanzia leo nisikuone hapa nyumbani kwangu umbwa we ,mchafu mkubwa usofunzwa na mamayo ufunzwe na ulimwengu,kwenda zako huko”.


mzee talenter akaingia ndani na kuchukua nguo mbili tatu za boga  akamrushia kisha akamwambia “toka…toka..toka…,usirudi tena na wala nisikuone tena hapa ntumbani nenda huko huko kwenye makundi yanayo kudanganya mtoto umejaa laana wewe,


Tangu kufariki kwa mamayo miaka mitatu iliyopita ,umepangaruka akili hata kwenda shule unaona kama ni kazi kubwa sana,unashinda mitaani kijana mdogo wa kidato cha nne hupendi kujifunza hufahamu ya kwamba elimu haina mwisho……unaipuuzia elimu ondoka  haraka nisiione sura yako iliyo komaaa utadhani mbuzi”.




Boga talenter   alikuakijana mrefu, Mwenye umbo pana nene lililojazia kwa sababu ya  mazoezi ya viungo aliyozoea kuyafanya kila siku chumbani kwake.ila ukimwangalia alivyopaa hewani unaweza  ukadhaniani ni  mtu mzima Mwenye umri wa miaka 35 kumbe ni mwili tu unaomsumbua,alijariwa sura nzuri yenye utanashati wa kumvutia kila mwanamke mrembo au msichana mrembo ingawaje alikua na nyota ya mvuto vijana wenzake wengi mtaani pao walimchukia na kudai kuwa hapendi kujiweka safi kimwili  kwa kifupi vijana wenzie walimfananisha na nguruwe vile.


Boga akaondoka pale Nyumbani kwao UBUNGO KIBANGU mtaa wa makoka,akiwa analia chozi lililoambatana na  maumivu  ya sikio pamoja na maumivu ya goti alilokua anatembea akiwa anachechemea,ingawaje watu wengi walimwona walibakia kumsikitikia tu kwa jinsi alivyo onekana,lakini hawakuweza kumsaidia kwani alikua na speed  kari utadhania ndege ya AIR TANZANIA, akakatiza barabara kadha kutoka kibangu kwenda ubungo akapita mawasiliano toure akavuka kanisa la mchungaji kakabe la full gosper bible fellow ship ,akatokezea mlimani city akajivuta zaidi eneo la soko  la mwenge Sasa akapunguza speed na kuanza kutembea taratibu akihema kwa kasi ya  ajabu kwani alikimbia speed nyingi na ukitegemea kutoka ubungo kibangu kwenda mwenge ni kilomita kadha, akajipereka mbele zaidi hapo akafika eneo la bamanga.


Boga akajivuta vema kwenye chuo kidogo cha maendereo ya jamii karibu sana na kituo kikubwa cha televisheni cha TBC, huko akabadirisha nguo zake chafu kishaakavaa zile safi ingawaje zilikua chakavu chakavu ukitegemea halishindwa kuzitunza vema kwa vile hakuwa na mazoea ya kuweka mavazi yke mahali pa safi,akajiingiza kwenye kikundi cha vijana waliokuwa wanachukua fomu za talent show.


Nayeye akachukua fomu zile kisha akamsogelea binti mrembo aliyejitambulisha kwake kwa jina la PAMERA,binti alikua amevaa mavazi ta gharama kiatu kikali haswa kama sio cha laki tatu basi ni cha laki mbili na nusu,mkoba alioubeba ulidhihirisha ya kwamba kuna kiasi kikubwa sana cha pesa ziko kwenye ule mkoba kulingana na mwonekano wake jinsi alivyoonekana pamera alionekana kama anatokea kwenye familia moja inayojiweza kifedha.


Boga talenter akamwambia pamera samahani sana sister utakapomaliza kuitumia pen yako naomba unisaidie na mimi nahitaji sana.pamera akamwangalia boga talenter kuanzia juu ya nywele  za utosini mpaka chini ya miguu yake  kisha akatabasamu tabasamu  pana lililoashiria furahaa fulani ya ghafla ingawaje boga talenter akujali ilo kisha akamwambia nitakusaidia nikimaliza kuandika.


Boga talenter akasubilia mpaka hatua ya mwisho aliyochukua pamera ya ujazaji wa ile fomu alipomaliza akampatia boga talenter ile pen yake aina ya spidor nyeusi boga akiwa hana ili wala lile alienderea kujaza  ile fomu ,lakini pamera alienderea kumwangalia kwa jicho la husuda na tamaa ya kumpenda.




Lakini katika kumtazama tazama boga talenter pamera akaiona michirizi ya damu nyepesi  kwenye got la boga,pamera akashtuka kdogo kama vile ametetemeshwa na umeme,akamuuliza boga ni nini kimemsibu mpaka michirizi ya damu ile  boga akamtazama pamera lakini akashindwa kujibu,pamera akaiona michirizi mingine ya damu pembeni ya sikio la boga,macho ya boga yalionesha kutoa machozi ingawaje macho yale mekundu hayakudondosha  hata tone la chozi.




Pamera akapata mwanga kuwa mvulana yule Mwenye sura ya kiutanashati atakua anahitaji msahaada wa haraka sana iwezekanavyo.Baada ya kumalizia ile kazi yao ya ujazaji wa fomu za mashindano talent show  wote kwa pamoja waka submitt zile fomu pamera aliyekua na gari  lake aina ya MERCEDENZ BENZ nyeusi, akamchukua boga talenter akamwambia amfuate hospitarini jambo ambalo boga talenter hakulipinga.


Alipokua anatembea kwa kuchechemea vijana waliokua wanachukua fomu baadhi yao waliziba midomo yao na pua zao kwani harufu kari ya kwapa pamoja na domo la boga liliwachechefua achilia mbali mwili uliojaa mapere mapunye na makovu yasoeleweka chanzo chake ni nini.


Boga kwa uchafu aliita fora hata mara kwa mara alifukuzwa shule ili awe msafi lakini hakujirekebisha.


Pamera akamchukua boga mpaka hospitary kubwa ya muhimbili,huko boga akapewa matibabu yote ikiwemo ya kurekebisha goti lililopinda na kuzuia kutoka kwa damu kwenye sikio lake na kwenye goti lake.


Lakini kabla ya hapo pamera alimpatia boga talenter first aid kwa kumsafisha vizuri goti na sikio, kumtia dawa aina ya spirt na kumfunga kwa kutumia bandage sehemu zote mbili sikioni nagotini,ndipo wakaelekea hospitarini kwa ajiri ya uchunguzi na matibabu zaidi na walipomaliza kupewa huduma zote za kitabibu pamera akagharamia kiasi cha shilling elfu hamsini hao wakaondoka zao.


Sasa pamera na boga taratibu wakaanza kuzoeana ,pamera  yule binti Mwenye umri wa miaka ishirini na miwili,mrefu mnene kiasi mweupe Mwenye rangi ya chungwa lililoiva, alijazia hips,matako yake mazito mfano  wake hakuna, achilia mbali mguu wake wa bia ulo watamanisha sana  vijana wengi wa kiume pale MAKONGO HIGH  SCHOOL,alikua ni binti wa geti kari aso patikana kwa uraisi.


Binti yule mrembo sasa  akazidiwa kwa matamanio yake kwa yule kijana mchafu ingawaje mtanashati,pamera akamtwaga swali boga talenter;


“vip unaye mpenzi wako wa kukuriwaza”.boga akajibu akiwa na  aibu usoni pake


“ la asha!! Sina”


pamera akamuuliza tena;


“ kweli huna”.


  boga akatikisa kichwa chake ikiwa ni ishara ya kuhafikiana na  lile swali,pamera akamwambia boga;


“ naitaji uwe wangu wa moyoni”.


 boga akacheka na kujawa na aibu usoni baada ya dakika chache akasema;


“ hamna noma sister hata mimi nime kuzimikia haswa”.


 Oooosh……… pamera aliyekua anaendesha gari akapumua pumzi nzito iliyoambatana na harufu nzuri ya marashi yaliyonukia mwilini,alifurahi sana kukubaliwa ombi lake  walipofika mataa ya ubungo pamera akasimamisha gari ili taa za kuruhusu magari ziwape nafasi ,kisha akamsogerea boga na kupiga busu la shavuni akatamka neno moja la kimahaba  I LOVE YOU BOGA boga naye aliyekua anachekacheka akajibu ILOVE YOU PAMERA.


Pamera akamuhuliza boga ni wapi anapoishi  boga akamwelekeza njia ya ubungo kibangu gari iliporuhusiwa kupita pamera akalitoa gari lake moto moto huyo  akakata mitaa miwili mitatu kisha wakawa wamesha wasili Nyumbani kwa wakina boga talenter.gari ilipofika Nyumbani kwa wakina boga talenter pamera alishuhudia nyumba ikiwa ni chafu haswa kila eneo  hali iliyomfanya pamera ajiulize maswali inakuaje nyumba ni chafu namna hii je wanaishi watu mahari hapa maswali yalilindima kichwani mwake paso majibu.


Akakaribishwa ndani ndani namo mlimstaajabisha sana kwa uchafu wa namna ile ila kwa vile yeye ni mwanamke na kwa asilimia kubwa wanawake wanapenda sana suala la  usafi.


Akamwambia boga anaitaji kupaweka mahari pale pawe safi na penye mvuto. pamera akawaita vijana wa kike watatu pamoja na vijana wa kiume wawili kwa njia ya simu yake ya mkononi,vijana wakawasili kama walivyo mwahidi kufika mapema,kazi ya kuipamba ile nyumba ikaanza .chap chap kama vile mashindano ya farasi wakimbiavyo,vijana wakaisafisha ile nyumba vizuri wakapanga kila kitu mahari pake, wakafyeka zile nyasi ndefu utadhania nywere za wanawake wa asili ta kiasia yaani wahindi.






Bahada ya kumalizia kushirikiana vizuri katika kuipamba ile nyumba pamera akawalipa wale vijana posho zao,vijana wakamshukuru sana wakamweleza kuwa iwapo akiwahitaji tena wao wapo tayari kwa msahada atakaohitaji .


pamera msichanma yule aso aibu akamsindikiza boga talenter  bafuni huko akamsafisha vizuri  mpenzi wake, kisha akamtaka waende shopping hao wakaerekea   MADUKANI BOTIQUE huko akamsasambulia viwalo  special,viatu vizuri pea tatu,laba za ngozi pea mbili,shirt tatu  za kitambaa cha sufu,tshirt  tatu pamoja na trouses tatu zote aina ya jeans.


Bibie huyo Mwenye huruma zake akampeleka boga talenter BARBARING kunyoa nywele zake ili kichwa kiwe swaafi boga akapenderea style ya kiduku style inayopendwa sana na vijana wa kisasa wanaojiita MASHAROBARO  au wasafi classics maana safari hii boga naye alikua msafi hasa,pamera aligundua kuwa boga talenter hana pocket money akaingiza mkono wake na kutoa burungutu la pesa  tasilimu shilingi million moja akampatia mpenzi wake mpya boga talenter,boga alifurahi sana shukrani alizozimwaga  boga zilikosa kuhesabika alimshukuru sana pamera akamwona kama ni mkombozi wake.bahada ya manunuzi yale pamera akamrudisha Nyumbani boga talenter akamuaidi kuja kumchukua  siku iliyofuata.


Pamera alikua ni binti wa tatu katika familia ya  Mr and Mrs Patrick ludoslovic ludwing na katika familia yao walizaliwa wote wakiwa ni wasichana dadaye wa kwanza aliitwa penslavia dadaye wa pili aliitwa penielia na yeye pamera alikua ndio kitinda mimba  katika familia ile.Babaye pamera alikua anamiliki kampuni yake ya kununua na kuuza magari ina ya PAJERO,LAND CRUISER,MITSUBISH,LAND LOVER,TAX,MERCEDENZ BENZ,TRECTORZ,BAJAJI na Mapiki piki aina ya TOYO na  BAJA.Mbali na kuuza magari pia alikua na biashara yake ya kuuza na kununua madini aina ya  GOLD,DIAMOND  na TANZANITE,ndio hizi biashara zilizompatia pesa na umaharufu jijini Dar es salaam kwani watoto wake walisoma vizuri,walikulavizuri,walivaa vizuri ,walihishi kwa fahari sana tofauti na familia nyingine nyingi  za majirani waliowazunguka.




Mamaye pamera alipenda sana kujushughurisha na shughuri mbali mbali za kiuchumi lakini babaye pamera Mwenye asili ya watu wa  ROMA ITALIA ,alijawa na kaji wivu kidogo hivyo hakumruhusu mkewe kujishughurisha na kazi za biashara zaidi ya kukaa tu na kustarehe.


Pamera na wazazi wake waliishi kwenye jumba la kifahari sana kwani jumba ilo lilikua ni ghorofa tatu na kila kitu kilikuwepo ndani,kuanzia wafanyakazi, walinzi pia huduma za DISPENSARY   yao wenyewe ilikuwepo.


Mchana ule babaye boga akawasili Nyumbani kwake akakaribishwa na harufu nzuri ya marashi aina ya PERFUMER JELLY  kwanza alistaajabu kuona nyumba yake imebadirika ghafra ,kwani hakutarajia kuyaona yale mabadiriko,taratibu akajongea mpaka ndani huko akasikia sauti ya kinanda ikitoa music mwororo,walipokutanisha macho wote kwa pamoja wakatabasamu boga akaanza kuimba wimbo wa siku maalumu ya kuzaliwa babaye maana siku ile ilikua ni siku maalumu kwa ajiri ya kuzaliwa babaye,


                            Happy birth day to you,……happy birth day to you,


                            Happy birth day dear father,……happy birh day toyou


                          How old are you……..how old are you


                       How old  dear father…….how old are you.


Alipomaliza kuimba ule wimbo haraka haraka boga talenter akaamka kwenye kiti alicho kalia akamsogerea babaye akamkumbatia naye babaye akamkumbatia pia wote wakawa ni wenye nyuso za furahaa iliyo kuu.Babaye akamwambia boga talenter  mwanangu mbona umenifanyia supprisment ya nguvu namna hiyo nyumba imebadirika ghafra,boga hakujibu kitu ila tu almwabia babaye


               “Dady ….,dady .umesahau kwamba leo ni siku yako muhimu  ya kuzaliwa”.


Dady akasema


“haloow!!!  thanks so much my son”.


basi dady akaisogerea ile meza,wimbo wao ukaenderea safari hii waliuimba kwa Kiswahili.


               Kata keki tuleeee……..kata keki tuleeeeee


               Kata keki dear dady…….kata keki tuleeee


Dady akakata kipande cha keki akamlisha boga naye boga akafanya hivyo hivyo akamlisha dady.baada ya furahaa yao kurindima boga talenter akamsimulia babaye  mwanzo mpaka mwisho jinsi alivyo kutana na pamera kwenye mashindano ya talent show,jinsi pamera alivyo mtongoza boga mpaka kuja kufanya usafi wa nyumba pamoja na kumpeleka shopping ,hakusahau kumweleza kuwa ni huyo huyo pamera aliyem peleka boga talenter hospitary ya muhimbili.


Mzee talenter alifurahi sana  maana alijua kua sasa mwanawe anaelekea kuwa kijana mtu mzima,pia yale mabadiriko ya harakaharaka yalimvutia sana mzee talenter alimpongeza sana mwanawe akamtaka awe na juhudi zile zile kila  apatapo muda  na nafasi,pia alimtaka mwanawe kuzingatia masomo ihari alimruhusu kwenda mashindano talent show




       -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------


Itaenderea toleo jalo……usikose tuwe pamoja

No comments:

Post a Comment