Monday, March 24, 2014


SURA  YA  TATU


                 BOGA TALENTER ANAFURAHI PAMOJA NA PAMERA


Baada ya kuisha kwa kazi ile ya mapishi vijana waliosalia walaanza kupongezana  kwa kazi nzito waliyo ifanya.siku ile pamera alimchukua boga talenter  akaenda kumtambulisha kwa wazazi pamoja na ndugu zake kama ni rafiki na mchumba wake mtarajiwa kwani kabla ya hapo aliwaambia wazazi wake kuwa amepata  rafiki mzuri ambaye angependa aje kuwa mume wake siku za usoni. Wazazi ndugu marafiki na jamaa ya pamera wakafurahi sana kumuona  boga talenter kwani alikua ni kijana mzuri haswa .penielia na penslavia  dadaze pamera wakaanza kuonesha jicho la husuda.


Roho ya kumtamania kijana yule ilikua kwa kasi kwani boga talenter kwa utanashati alikua yupo juu kwani katika wanaume vijana ishirini ambao wangepita mitaani pamoja na boga talenter hakika mtu aliye watazama asingesita kumsifia boga talenter kwa uzuri na utanashati.ni jina tu  alilopewa la boga ndilo halikumpendeza ila kwa utanashati kijana aliita fora hata babaye usiku na mchana alijitwanga maswali yasiyo na majibu ni wapi mtoto yule alikouta  hali ile ya kuwa bonge la handsome.


Boga naye akamtambulsha yule mrimbwende pamera kwa   kwa babaye mzee talenter aliyekuja muda mfupi baada ya mashindano kuanza,wote kwa pamoja walitawaliwa na nyuso za furahaa ya ajabu.


Siku ile pamera aliona kuwa uchovu ni mwingi sana ndani ya mwili wake kwani kazi waliyoifanya ilikua ni kazi nzito na ya kufa mtu,akamwomba boga waende ufukweni mwa bahari ya hindi  kujipumzisha .huko nako walipofika michezo mbalimbali ilienderea mchezo ambao ulikua ni mgumu sana kwa boga ulikua ni kuogelea boga hakujua kuogelea hata kidogo alipata shida sana ya kucheza na maji pamera alipoona udhaifu ule wa boga akaanza kumfundisha taratibu kwa kutumia mipira maalumu ya kuogelea na maboya ya gari hali ambayo boga talenter  alifurahia zaidi.


Jioni ya siku ile pamera alimpeleka boga sehemu nzuri ya MLIMANI CITY CINEMA  ili kucheki muvi firamu na tamthiriya, sinema iliyo mvutia sana boga talenter ni sinema ya marehemu STEVEN CHARLES KANUMBA ilitoitwa  ANKO JJ kwani msanii aliwakonga sana  mioyo watazamaji kwa kipaji chake alicho kionesha jioni ile wakacheki  tamthiriya moja ya kikorea iliyo kwenda kwa jina la  JUMONG na wakamalizia kwa firamu tamu ya mwana dada aliye chipuka kwenye muvi ya FOOLISH AGE wala si mwingine bali ni ELIZABETH MICHAELI au LULU.


Achilia mbali kumpeleka  boga talenter sehemu nzuri ya mlimani city cinema  binti yule wa tajiri  alimpeleka boga talenter hoter moja yenye hadhi Ya kimataifa  inayoitwa NYUMBANI LODGE  hoter ya mwanamuziki wa kimataifa LADY JAY DEE. Wakaagiza supper ya kinywaji cha maziwa mazito CAPPUCCINO kwa utamu ule hata boga aliona  ajirambe mikono kama mtoto mdogo kwani hakuwai kuonja vitamu tamu vya hoterini,baada ya supper yao kuisha wakaagiza na dinner iliyo sheheni wali kwa kuku wawili wazima pamoja na juice ya  ya matunda.


Siku ile kulikua na ugeni  wa wanamuziki   kutoka mwambao MZEE YUSSUPH na ISHAA RAMADHANI almaharufu kwa jina la ISHAA MASHAUZI , wanamuziki wale wa nyimbo za TAARABU walitumbuiza nyimbo zao zilizo wakonga watazamaji kama vile MAMA NIPE RADHI.ukumbi wote ulibakia kupiga kelele za nderemo na vifijo sio isha mashauzi tu na bendi yake ya mashauzi classics pia mwanadada lady jay dee akiwa na bend yake ya machozi aliwapagawisha  wapenda starehe kwa wimbo wake wa YAHAYA. Hakika siku ile ilikua ni siku  ya burudani tosha kwa  vijana hawa wawili.


Usiku mnene ulipoingia pamera akamwomba boga talenter wakodishe chumba hoterini ili walale pale pale lakini boga alisita kwani hakumwaga babaye mzee talenter hivyo aliingiwa na hofu kuwa mzee wake anaweza kumtafuta  kuwa na wasi wasi na mahari alipoenda boga talenter.


Pamera akamrudisha boga talenter Nyumbani kwao kisha na yeye akarejea Nyumbani kwa wazazi wake  ilikupumzisha kichwa ubongo na akili  kwani mc masanja aliwatangazia washiriki kuwa walitakiwa kujiandaa na shindano jingine bab kubwa la fashen show baaada ya siku tatu zijazo

No comments:

Post a Comment