Wednesday, October 21, 2015


MWANAUME UYAKAVA MADHAIFU YA MWANAUME  MWENZAKE

Katika suala la mapenzi wanaume wengi sana wana madhaifu kwa mfano,kushindwa kumjali,kuympenda kumthamini,na kumheshimu mwanamke aliye naye,sio tu hivyo hata katika suala la nguvu za kiume,wapo wenye nguvu nyingi na wengine madhaifu,wapo walio teke teke na pia wapo wasiojua kitu yaani ziro power ziro percentage.

 

Sasa Elaija

Wanaume wengi hudanganya mambo mengi tu lakini hawapo tayari kukuambia kuuhusu kipimo au ujazo wa nguvu zao,wengi hujigamba kwamba wao ni strong powerfull na wenye nguvu,hivyo mwanamke hukimbilia popote ili kupima madhaifu ya mwanaume na mwanaume mwenzie

Elaija

Usikubali jambo kama hilo likutokee maishani mwako,

Be strong ,jiamini,take care be always care fully and love you

 

 

 

MAGELIA

Elaija

NIMEKUA NA RAFIKI YANGU WA KIKE KWA MUDA WA MIAKA MITATU

LAKINI HATUJAPATA KUONANA SANA SANA TU,

HATUJAPATA KULALA PAMOJA,

HATUJAPATA KULA AU KWENDA AU KUNUNUA VITU KWA PAMOJA,KWA UPANDE WANGU NIMEKUA DHAIFU SANA KWENYE MAPENZI, MAGELIA AMEKUA MKARI SANA KWANGU, AMEKUA  NA HASIRA SANA KWANGU, HATA SIKU MOJA ALITOROKA KWENDA MORO GORO, yote ni kwa sababu ya mapenzi

SASA AMENINUNIA ANADAI TUACHANE ANADAI PENZI LANGU NI UPEPO,NA ANAHITAJI UHURU WAKE,ANAHITAJI KUA NA MWANAUME WA KUMLIWAZA.NIMEYAONA MADHAIFU YANGU LAKINI PIA SITAKI KUMRUHUSU ANIACHE

NAMPENDA SANA MAGELIA,JAPOKUA NIMEKUA DHAIFU SANA,NIME MWAHIDI VITU VINGI SANA, SASA AMECHOKA ANAHITAJI UHURU WAKE,JAPOKUA ALIKUA ANA UPENDO MWINGI KWANGU LAKINI HILI NALO LINANITIA WASI WASI NAHUMIA SANA IWAPO ATANIACHA NAMPENDA SANA MAGELIA

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

ASILIMIA KUBWA YA WATU WANAOTIZAMA MPIRA  NI WANAUME

Elaija

Mchezo wa mpira ni mcezo unaopendwa sana katika mataifa mengi sana duniani,ni mchezo unaovuta maelfu ya watu kwenda kuutizama na pia wana furahi kuona pande mbili zinagombana.ili ziweze kupata ushindi.

 

Elaija.

Siku moja nilienda kutizama mashindano ya mpira kati ya mbeya fc na timu Fulani ngeni kama sikosei iliitwa mtibwa sugar,nilipoingia kwenye ukumbi wa sokoine niliona kundi kubwa la wanaume wanafurahia mpira …..lakini nilipotizama pande zingine niliona wanaume wachache sana kwa kiasi kikubwa nilijisemea moyoni mwangu

           ,,mpira ni mchezo unao wavutia vijana wengi wa kiume,,

 

 

DUU!!!! ULEVI NOOOOMA.

Ulevi ni kitendo cha kunywa  kiasi Fulani cha pombe,unaweza kunywa kwa kiasi Fulani au kuzidisha mpaka ubongo ukakosa ufahamu.

Lakini Elaija

 

Matokeo ya ulevi huo ni kushindwa kuinuka kimaendereo,au kuzorota akili na kushindwa kufanya kazi ipasavyo matokeo yake wahusika  au mhusika uwa tegemezi.

Elaija

Pombe ina gharama zake,pombe inaweza kukufanya ushindwe kueleweka,katika jamii inayo kuzunguka,tazama ulevi ni kitendo cha kutumia madawa ya kulevya na madhara yake ni kifo au kupata ajari au hata ugonjwa wa kansa.

 

Acha ulevi jenga nchi leta maendereo

 

MAISHA YETU NI KUFANYA KAZI

Kazi ndio maisha yetu yanahitaji mtu awajibike kisawa sawa,usiku na mchana vijana wana waza kazi,umasikini unatutawala kwa vile hatuna kazi na pia njaa inatunyanyasa eti kwa sababu tu hatuna kazi..kazi ni kituy bora sana katika maisha yetu kitu kinachoweza kutufanya sisi tukajenga maisha.

 

Any way nawatizama vijana wanavyo chakarika mikono yao au miguu yao,migongo yao ina wahuma lakini pia wanajitahidi tu kuwajibika,wanajitahidi tu kuteseka,japo kupata ridhiki yao maisha ni ni magumu.

 

Vijana hao ni wazuri sana hakika wana nivutia maumbo yao,maumbo yao yamejengeka kwa sababu ya kufanya kazi wana hangaika siku zote ili wapate kufanikiwa.hakika kazi ndio msingi wa kujenga nchi,

Nchi masikini haiwezi kuenderea kwa kutegemea misahada ya mataifa mengine au wafadhiri pasipo kufanya  kazi

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

AMEKWISHA ONA SASA NI KUMWACHA TU

Binti sasa amekua,matiti yamechomoza yamekua mazito hakika yana mvuto, wowowo lake sio dogo,yaani ni kabichi au tikiti maji,mh!!linaenderea kunesa nesa ana tabasamu zito na mikono yake na mapaja yake pia ni mazito..

 

ELAIJA, nikwambie kaka yangu

Sasa ameshapendwa mmh!!! Mmh!! Jamani au amesha kulionja tunda? Mmh ndivyo sukari ilivyo utamu wake ni kuonja kidogo kidogo…..ah ah ah no  ..utamu wake ni kuweka kwenye chai.

Elaija umeona eeeh!!!

Ameshakuonja na anatoroka nyumbani kwao mmh!! Analala mbali na nyumbani kwao mmh amekatazwa lakini mbona hasikii?

 

Some time am    ekua ni mtumwa wa mapenzi,kwa sasa ni mjamzito eeeh!! Amezaa lakini bado anaenderea tu na tabia yake ya kupenda penda eti kwanini jamani? Au ndio mahitaji ya kimwili yalivyo

 

Mmmh!!! Ameona na sasa ni kumwacha tu.

 

 

Elaija mbona una ona  aibu

Elaija  inakuaje mbona unapotembea  waogopa!!mmh!! kwanini elaija

Woga utakumaliza,woga utkuponza na woga hautakupeleka mbali,woga na aibu ni vitu viwili visivyo na tofauti,

 

Sasa Elaija

Jitahidi kuukwepa woga,utupilie mbali woga,uambie woga kaa mbali na mimi hauna nafasi hata kidogo kwenye mwili wangu..

Elaija

Hatuna muda mwingi sana wa kuishi duniani,miaka tuliyonayo ni michache,sana na pia tumebahatika nafasi tu ya kuliona jua mwezi na nyota nyota pamoja na vyote menyezi mungu ametupatia.

 

Elaija jifunze vyote ili viweze kukusaidia maishani.wala usiwe na woga Elaija jitahidi tu kupitia hata kama ni vigumu.

 

Love you Elaija

 

 

 

 

NATAMANI NINGE KUA MUNGU

Elaija

Dunia imeumbwa kwa ufundi,utaalamu,ujuzi na kipaji cha hali ya juu zaidi,ambapo hakuna awezaye kufanya  mambo mazito kama yale ayafanyayo mwenyez mungu.

 

Elaija

Popote utakapopita chochote utakachoona au lolote utakalo sikia,jiulize hivi hizo nguvu zimetoka wapi,Elaija just remember mungu alipo kamilisha kila kitu kiwepo duniani ndipo akamleta binadamu aweze kua ni mtawala wa hiyo dunia.

 

Elaija nikwambie

Na mimi natamani sana ningekua mungu mkuu mwenye nguvu zote,japo niweze kuitengeneza dunia na vyote vilivyomo,natamani sana tenasana kumuumba binadamu natamani zaidi lakini udhaifu wangu ni kua sina hizo nguvu

 

Any way najisemea moyoni mwangu upendo wa mungu unifunike ili niweze kutendaz yale yote makuu ayatakayo mwenyezi mungu niyatende……….

 

 

Nahitaji kubadirika

Nimeyapima sana mawazo yangu,nimeyapima sana nimeyapima kwa muda  mrefu,nimeyapima kuanzia mwanzo mpaka hatua ya mwisho na hatimaye nikaja kugundua,udhaifu na upungufu wangu katika suala zima la kufikiria namna gani naweza kupambanua ili niweze kuchochea na kuyaleta maendereo.

 

Na jawabu  nililolipata ni kua nina haja ya kubadirika,nibadiriken ili niweze kujivunia maendereo na maendereo yenyewe inanipasa niyatafute kwa majasho makubwa na makari mno,ndoto zangu hazitakuja kutimia iwapo nitashindwa kutimiza mipango na matarajio na hapa nimeona mbali sana ya kwamba iwapo nitafanya uzembe  nitashindwa kutimiza yale yote niyatarajiayo.

 

Kila siku nimekua nikilalamikiwa ya kwamba sina maendereo au sitakuja kua na maendereo ya haraka,heshima yangu  imeshuka ana kupungua kwa kiasi kikubwa sana,nimekua ziro kwenye kila idarasina biashara sina mtaj wala sina maana yoyote ile.

 

Na sasa nahitaji kubadirika nahitaji kutafuta pesa au mkopo nijikwakwamue,

Ili na mimi japo niipate nahafuu ya maendereo.

 

 

 

 

 

Imekufa  lakini inaishi hai

Ndio  kwa mtazamo wangu  nahualisia wamaisha yao wao ni watu pia wako hai na uhai wao ni ule uhai unaotokana na tamaa zao za kuvipata vile vyote vyenye anasa na tamaa za kidunia

Kwa mfano walipokua hai wanaishi duniani walitamani sana kua na nyumba nzuri ,magari mazuri ya kifahari,pesa nyingi,wanawake pamoja na watoto wengi tena wazuri,tama yao ilikuwa kubwa na nzito       sana lakini ubaya wake hawakuvipata vyote hivyo walivyovitamani,sikatai nikikwambia ya kwamba kuna baadhi ya vilivotamaniwa walivipata lakini ukweli wa mambo unasema kwamba hawakuchuma vingi.Hapo ndipo walipoweka fikra zao mbele kwa mbele,wazee hawa wakaapa kuwa wakifa tu ni lazima wawe nusu hai nusu wa wafu nani lazima mali,utajiri,fahari na vyote wavitakavyo watavipata tu

Wachambuzi wa mambo haya wameshasema kinagaubaga kuwa hawa waliokufa sasa wanafurahia maisha yao huko   kuzimu,kwani wanazo nguvvu za kutosha kumteka  binadamu kimawazo kifikra,kiuchumi,kisiasa na kiutamaduni,

Ndio wameweza,wanawatumia waganga wa kienyeji ,wanatumia watu,wanyama na  wadudu  ili kutimiza dhima zao wameungana na majini,mapepo au mizimu ili kutimiza adhima yao kwa mfano iwapo wewe unashida shida yako ni ugonjwa utakao gharimu laki mbili uwaendeapo watakwambia utafute milioni tano ili upone kwa kweli ndugu yangu unaitafuta sana hiyo million tano ili upate  unaafu ,matokeo yanaweza kuwa chanya au hasi, utapona au usipone na usipopona hasara kwako ndugu yangu  na mwisho wa yote wao hufurahia mali na utajiri wao

Ndio hao wamekufa lakini wapo hai wanapumua lakini pia hawapumui muda firani wa maisha yao wanakunywa pombe na damu ya binadamu  na pia wanatoa ahadi kibao za kumtajirisha au kumnufaisha mwanadamu na matokeo yake mtu hupata hasara ya kimaisha   ndio haowalio hai na wafu kwa jina lingine  wanaitwa mizimu

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

ASANTE YESU

 Asante yesu ndio maneno niyatamkayo moyoni mwangu siku ya leo asubuhi pamekucha salama mimi ni mzima wa afya tena afya njema ,afya bora nimeliona tena jua ,nimeona mwanga wa asubuhi moyo umejawa hamu za kuimba nyimbo mbali mbali  za  kidunia nimejikuta  nina imba  moyoni mwangu  ‘’najisikia kuweweseka ,najisikia kuweweseka ‘’ najitahidi kuimba taaratibu moyoni nimejazwa amani na furaha ,sijui kwa nini leo.

Lakini leo nimekumbuka kwamba nahitaji kubadilika  nahitaji kufanya mapinduzi  na mapinduzi yenyewe yawe yakuni toa kiuchumi,nahitaji kujikwamua kutoka kwenye umasikini,ufukara na hali mbaya ya kimaisha,ili na mimi niwe miongoni mwa wale wenye heri maana mawazo yenye heri  yanatoka kwa mungu nani mawazo mema yenye faida

 

Mungu anibariki sana

Ninaifanya juhudi.

 

Bissmillah wadudi,kukusifu sina budi,

Mola wangu saidi,nitafanya na juhudi,

juhudi na makusudi,heri zilizo jaa sudi,

ninaifanya juhudi,

 

uwe wewe shaidi ,kunako kiti cha jadi,

ukinikinga na radi,maadui na maasidi,

nifanye zangu juhudi,hima hima hima,

pole pole ndio mwendo,

 

iwapo nimekopa mtu,au nimeazima kitu,

kurudisha isiwe katu,kuvirejesha vya watu,

kwani wema wa kibantu,hauhozi kamwe katu,

kigagulo cha kuazima……….

 

Nisiwe na roho jitu,lenye sumu kama chatu,

Nikatengwa nao watu,nikatupiwa misitu,

Bora nifanye juhudi,toka mbeya mpaka mwanza,

Asha sitakufa moyo!!!!!

 

Iwapo mehaidi jambo,”promise ‘’yenye vitendo,

Nisije haribu mambo,siasa napiga kipondo,

Tafanya si majigambo,ni vitendo vile vya jando

Sitoweza pata kikumbo heshima langu kulinda,

 

Napigana nafsi na umbo,vyote kuvifanyia lindo,

Kwenye milima mabonde,ntajipiga moyo  konde

 

 

 

 

 

 

 

 

 

UKWELI WA MAMBO

 

Kwa sababu wewe ni binadamu kama binadamu wengine,imekupasa uyatende yale yaliyo mema na mema hayo yawe ni yale mema ambayo uyatenda wanadamu wenzako,yawe mema  au yawe matendo ambayo wao huyalilia kila siku.

 

Ikiwa wewe ulizaliwa ukala,ukanywa,ukaongezeka ukaupita ujana ukafikia kipindi cha kuyajua yapi yaliyo mema na yapi yasiyo mema na hivyo ndio itakavyo kua hivyo hivyo ata kwa watoto wako.

 

Utatamani kua na mwenzi wako katika maisha,kwa maana hiyo  basi utajaliwa kua na watoto au mtoto na hicho kizazi chako kitatamani kuyatenda yale ambayo wewe uliye tangulia umeyatenda….labda kinyume chake tuseme kuwa  baadhi ya mambo  kizazi chako hakijapata kuyatendaa.

 

Kama ulisoma,uliongea,ulifurahi au ulijiunga na vikundi mbali mbali vya kiutamaduni au vya kijamii hivyo basi tambua  kua hata mtoto au watoto wako,watafanya hivyo au wataenda mbali zaidi katika kuyatenda matukio mengi zaidi kulingana na wakati au kulingana  na hayo matukio.

 

sisi ni wanadamu tuna tama zetu tunahitaji kuyatenda yale ambayo ni haki kwetu na pia ambayo ndio msingi wa maisha yetu,tukijinyima tutakua tumezinyima nafasi zetu, na tumenyima muda wetu pia imetupasa tuwe makini na imara zaidi,kwani dunia inaweza kutupotosha kwa vitu vidogo vidogo tu ambavyo vinaweza kutuangamiza.

 

Yours

Elaija elia

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

TUMEPEWA VYOTE BURE.

Mwenyezi mungu amempatia mwanadamu maisha yaliyo bora zaidi,kwa jinsi ninavyofikiria kwanza nikiutazama ulimwengu jinsi ulivyo naweza kusema kua hatuna tulichopungukiwa,vyote tunavyo na vyote tumepaswa kuvitumia ili tuweze kuenderea na ili viweze kutusaidia,.

 

Hatuna tusichokua nacho vyote tunavyo na vinaidi kuongezeka,kila siku inayoitwa siku ya leo,achilia mbali ongezeko la hivyo vitu pia tunavyo vitu ambavyo  tumepewa lakini hatuvioni au labda tuseme vimejificha sana ulimwenguni.

Lakini mwenyezi mungu ni pendo pendo,pendo lisilo na mapungufu pendo la dhaati,pendo jema la asubuhi, pendo la mchana na jioni ni lile pendo lililoleta wagunduzi waganguzi, wenye vipaji na vipawa,ubunifu,ujuzi maharifa juhudi na elimu isiyo weza kuchuja,hata kama itachuja japokua ipo lakini pia itaenderea kuwepo milele na milele

 

 

Vyote vilivyojificha twaweza vigundua twaweza vitambua twaweza viona,kwa nguvu na kwa uwezo wake mwenyezi mungu jalia.ikiwa hatujaviona leo basi tegemezi letu ni kuviona kesho ikiwa sio kesho basi tutegemee kuviona kesho kutwa au siku yeyote ile,

 

 

Daima hatutakiwi kujisifu kuwa tu wajuzi sana,tukumbuke basi kua ikiwa mungu mwenyezi hajatuonesha  sisi basi anao mpango wa kuwaonesha wale au wajao au vizazi na vizazi dunia imeumbwa na vitu  vinavyoonekana au visivyo onekana…..dunia imeumbwa na kupewa mwanga pamoja na giza kwa kifupi basi tunajua kua mungu ametupa na wala mungu hajatunyima..

Wasalaam.

Wenu katika bwana

Elaija Elia

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

MBEGU YA MUNGU

MBEGU ILIYO BORA ZAIDI

NDIYO NGUZO IMARA

Mbegu iliyo bora ndiyo ile mbegu inayozalisha na kujaza dunia,pasipo hiyo mbegu bora ni vigumu kwa dunia yetu kujivunia kwamba nafsi yake ya kuongezeka itakua pale pale.

 

Mbegu hiyo ni mungu na mungu ndiye mbegu bora zaidi duniani,ndiyo mbegu inayo zalisha dunia ndiyo mbegu ambayo inajivunia, ndiyo mbegu ambayo pasipo yeye dunia au nafsi haiwezi  kuongezeka au kuwepo pale pale.

 

Daima wanadamu hujisemea wao ndio walio bora zaidi au wao ndio imara zaidi japokua wamesahau ya kwamba mungu ndiye bora zaidi aliyewaumba ndiye imara zaidi ominipotent god, god of ominisience, the powerfull world mighter,world qoncquarol since the beginning of human creature.

 

Daima siku zote mwanadamu ujigamba ya kwamba yeye ni yeye,yeye ni mtawala mfalme atakayeshinda vita vyote yeye ni nguzo imara,nguzo ya kumpinga adui yake,ingawaje ndio huyo huyo binadamu anaye weza kujua kua ni macho yake ndiyo yanayo weza kumuokoa au kumuweka katika hatari Frani. Akizubaa tu kidogo au  akishindwa kupigania nafsi yake basi hatari inaweza kumjia na hapo ndipo anapoweza kupoteza cheo chake sifa yake au utawala wake,ngazi yake,utawla wake au na vyote alivyo navyo.

 

Na jambo la msingi hapa ni kwamba kifo ndicho kitu kibaya zaidi kinachoweza kummaliza mwanadamu,yeyote Yule mwenye nyama nafsi,pumzi na damu,lakini pia ikumbukwe kwamba sio hivyo tu mbegu ya mwenyezi mungu itaenderea kuwepo milele na milele hata kama kifo cha mwanadamu kimetukia mwenyezi mungu ataenderea kuishi milele na milele.

 

Assalam allaykum

Na bwana asifiwe

Amen

Ndimi Elaija Elaia

 

 

 

 

 

 

 

NI VIZURI SANA KUFIKIRIA

Kabla ya kutenda yampasa mtu awe na fikra za kufanya uamuzi huo,lakini pia  ni vizuri kujua fikra hizo ni negative au posttive,fikra zitakua chanya pale mtu afikiriaro litakua ni jambo jema lenye kumletea faida,mabadiriko au hamasa Fulani ya kumletea maendereo,lakini pia fikra zikiwa negative uleta matokeo negative, yakiwemo yale ya kutaka kudhuru mwili wa binadamu kutusi,kuiba au jambo lolote lile hovu.

 

 

 

Hebu tuachane na hayo mambo ya negative and positive thinking,mimi mwenyewe nimejiwa na fikra nyingi kichwani mwangu,fikra zangu zinaniambia kua mimi sio masikini kama ninavyojidhania.mimi nimeajiriwa na serikari ni na uwezo wa kuazima benki kiasi cha pesa karibia milllioni kumi na tano kwa lengo la kufanya biashara ili nijikwamue na madhaifu ya uchumi na je nikishajikwamua  si nitaondokana na mazaifu yangu kiuchumi, na maisha yangu yatakua positive zaidi ya kuwaza negative…..

 

 

KWA VIJANA

Nikweli isiyo pingika kusema kua vijana wakiachwa mitaani bila ya kukombolewa huweza kufanya mambo mbali mbali yasiyo faa katika jamii na suala hili lina wafanya vijana kuonekana kama vituko au vitu vya ajabu ajabu katika jamii kivipi? Ni hivi wanahitaji kufanya kazi za kijamii kiuchumi au hata za kiutamaduni bila kusahau hamu yao kisiasa.

 

Namna gani?

Wameachwa mitaani,wengi wao hawana elimu,hawana pesa hawana chochote, cha kujivunia, kitu ambacho kitaitwa kitu cha kuleta maendereo na matokeo yake wamejazana barabarani hawana kazi hawana kipato hawana mali hawana chochote.na je mipango yao ni hipi kuiba kuvamia au kupora,kupiga watu kubaka au kufanya matukio mengi ya kutisha na ya aibu yasiyofaa eti sababu tu wameachwa,hawajitambui na wala hawana kazi za  za kuwatoa kimaisha

 

 

SIKU ZOTE MNAFQI HAJIKUMBUKI

Mnafqi ana sifa ya kupinga au kupingua, mnafqi ana sifa ya kukubali au kukataa Na matokeo yake Ni kwamba mnafqi hajikumbuki Na wala hakumbuki matukio au mawazo yake hujikuta ana paranganyika mpaka akili zake zinavurugwa.

 

Mnafqi ana sifa ya kushashia, kuropoka au kusereleka Na kubwabwajuka na hizo ndizo sifa pekee zinazoweza kumfanya mnafqi aonekane amepoteza mwelekeo.

 

Unajua mnafqi ana tabia moja hawezi kuyatunza yaliyo moyoni mwake,kwani apingapo jambo upande huu pia utetea  jambo upande ule ni sawa sawa na kusema yeye ni shabiq wa samba na pia ni shabiqi wa yanga hana upande mmoja mbadara anazipepea bender azote mbili hana msimamo na kwa bahati nzuri hadhira humjua tu kwa sababu ya kuparanganyika kwake.

 

Basi tukumbuke ya kwamba mnafqi hana kumbukumbu.

 

 

Nisijadiliwe

Nashangaa japokua sitaki kushangaa sanaa mpaka kufikia hatua ya kugeuka mwendawazimu,mjaa kasoro, kwanini mtu anijadili anastaha gani,sifa gani,mwelekeo gani, mpaka anijadili.mmh! leo kuna jirani yangu mmoja kaniambia eti mimi ni mbairi.

 

Sikua na hasira ila nilimfikiria vibaya kwani moyo wangu umeniuliza swali au maswali furani yaendayo,na malezi yangu.nimejiuliza imekuaje mtu huyu asiyejua nilipotoka ninapokwenda au nilipo anafikia hatua ya kunijadili na baya zaidi ana nisema kwa moyo wake wote.

 

Sitaki mtu kama yeye anijadili labda angekua yeye ni mzazi wangu hapo ndipo napaona ni sawa wazazi wangu ndio walionifikisha hapa nilipo wao ndio walionilisha,nivalisha,ninywesha nilaza na kunikuza kimaadili bila kusahau gharama zote za kielimu hawa hawanijadili au kunisema kimakosa iweje yeye  jirani yangu abwabwatuke.kwani yeye ni nani haswa au ndio uhuru wa kuongea chochote ulivyo…the!teh!teh!(nacheka mwenyewe)

 

No comments:

Post a Comment