Monday, July 1, 2013

MAGHANI

Zipo fani mbali mbali za maghani ambazo zimeainishwa katika tanzu mbili kuu:

Maghani ya Kawaida
Maghani ya Masimulizi

--------------------------------------------------------------------------------

Maghani ya Masimulizi
Lengo la maghani ya aina hii ni kusimulia kisa fulani, historia, n.k.

Kuna fani mbili za Maghani ya Masimulizi:
a) Tendi
Tendi ni ushairi mrefu unaosimulia matukio ya kishujuaa. Tendi zinaposimuliwa huandamana na ala za muziki.

Sifa za Tendi:

Ni ushairi mrefu
Husimulia matendo ya kishujaa kwa njia kishairi
Husimuliwa badala ya kuimbwa
Huandamana na ala za muziki
Husimulia visa vya kihistoria
Hutungwa papo kwa hapo

--------------------------------------------------------------------------------

b) Rara
Hizi ni hadithi fupi za kishairi zenye visa vya kusisimua, zinazosimuliwa zikiambatanishwa na ala za muziki. Aghalabu hughanwa na watoto; na hutumika kama michezo ya watoto.

Sifa za Rara

Ni hadithi fupi za kishairi
Husimulia visa vya kusisimua
Zinaweza kuimbwa au kusimuliwa
Huambatana na ala za muziki
Aghalabu huwa ni visa vya kubuni

--------------------------------------------------------------------------------


Maghani ya Kawaida (Sifo)
Maghani ya Kawaida ni maghani yanayosifia mtu, kitu au hali katika jamii

a) Majigambo au Kivugo
Haya ni maghani ambayo mtunzi hujisifia (kujigamba) namna alivyo hodari katika nyanja fulani. Tungo hizi hutumia chuku na maneno ya kejeli kuwadunisha wapinzani wa mtunzi.

Sifa za Majigambo

Hutumia nafsi ya kwanza
Msimulizi hutumia maneno ya kujigamba
Msimulizi hutumia chuku kwa wingi ili kujisifu
Hutungwa kwa ubunifu mkubwa na hutumia mbinu kama sitiari, vidokezi, ishara n.k
Majigambo mengi huwa mafupi, lakini baadhi yake huwa marefu.
Huwa na matendo matukufu ya msimulizi
Huwa na ahadi za matendo kutoka kwa msimulizi

--------------------------------------------------------------------------------

b) Tondozi
Tondozi ni aina ya sifo ambayo husifia watu mashuhuri katika jamii kama vile viongozi

Sifa za Tondozi

Huwa ni ushairi wa kusimuliwa
Husifia mtu mwengine, mtu mashuhuri
Hutumia chuku
Hutumia mbinu kama sitiari, vidokezi, ishara n.k
Hutaja matendo makubwa ya kiongozi anayesifiwa
Pembezi
Pembezi ni maghani ya kumsifu mpenzi.

Sifa za Pembezi

Humsifu mpenzi wa mtu
Aghalabu huwa ushairi mfupi
Hutumia tamathali za lugha kwa wingi kama vile ishara kusimulia umbo la mpenzi
Pembezi zinaweza kuandamana na ngoma
ii) Pembezi - tungo za sifa. Zinaweza kusifia kundi fulani la watu, wanyama, njaa, mvua, n.k

No comments:

Post a Comment